• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka Atoa Wito kwa Wafanyabiashara Kuzitumia fursa za Uwekezaji Kujiongezea Kipato

Posted on: December 31st, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Anthony Mtaka amesema mkoa huo utaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara ili waweze kunufaika na uwekezaji wanaoufanya ikiwa ni pamoja na kuchangia katika ukuaji pato la taifa.

 Mhe. Mtaka ametoa kauli hiyo katika hafla ya uzinduzi wa hoteli ya kisasa ya Sweet Dreams mjini Bariadi na kusisitiza kuwa wafanyabiashara wanapaswa kuzibaini na kuzitumia kikamilifu fursa za kibiashara zilizopo ili waweze kujikwamua kiuchumi na pia kuharakisha maendeleo ya mkoa.

“Mwaka 2019 mkoa wetu utakuwa mwenyeji wa matukio makubwa ya kitaifa, kutakuwa na Nane Nane, Maonesho ya viwanda vidogo SIDO, Jukwaa la Ushirika na Siku ya mifuko ya hifadhi ya jamii, kumbukeni matukio yote haya yatakuja na wageni wengi watakaohitaji chakula, malazi na usafiri, mmejiandaaje kuitumia fursa hii,” alihoji Mhe Mtaka.

Halikadhalika Mhe Mtaka amewasisitiza wafanyabiashara mkoani humo kuhakikisha wanatoa huduma zenye ubora ili kuvutia wateja wengi zaidi kutoka ndani na nje ya mkoa jambo ambalo amesema litaongeza hamasa ya kuutangaza mkoa wa Simiyu.

Aidha kuhusu ukuaji wa sekta ya viwanda, mhe Mtaka ameongeza kuwa mapema mwaka 2019 mkoa unatarajiwa kuanza ujenzi wa viwanda vikubwa vitatu ikiwa ni pamoja na kiwanda cha vifaa tiba kitakachojengwa katika wilaya ya Bariadi pamoja na upanuzi wa kiwanda cha chaki na ujenzi wa kiwanda cha vifungashio mradi utakaotekelezwa wilayani Maswa huku  akiwataka wafanyabiashara kuweka mikakati ya kunufaika na fursa hiyo.  

“ Ujio wa miradi yote hii  unategemea utayari wenu ninyi wafanyabiashara, endapo mnataka kunufaika na fursa zitakazojitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi hii fanyeni maandalizi mapema, mfano viwanda vyote nilivyovitaja vitaajiri watu zaidi ya elfu mbili na wote hawa watahitaji nyumba za kupanga, zitatakiwa hoteli na nyumba za wageni”, alisisitiza RC Mtaka.

Akijibu changamoto zilizobainishwa kwenye risala ya uongozi wa hoteli ya Sweet Dreams ikiwemo tatizo la maji pamoja na tatizo la kukatika umeme mara kwa mara, Mtaka ameuhakikishia uongozi wa hoteli hiyo kuwa serikali inazishughulikia  ikiwa ni pamoja na kuhakikisha utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa Lamadi unakamilika kwa wakati na pia  amewahakikishia kuwa maandalizi ya kujenga kituo cha kupozea Umeme kitakacho maliza tatizo hilo yamekamilika.

Kwa upande wake mwenyekiti wa wafanyabiashara wa mkoa wa Simiyu ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Itilima Mhe.Njalu Silanga amesema umoja huo utaendelea kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano zinazoweka mazingira rafiki ya kufanya biashara akitolea mfano uamuzi wa serikali ya mkoa kuruhusu biashara kwa saa 24.

Kuhusu ushiriki wa wafanyabiashara kuchangia pato la taifa kwa kulipa kodi, Njalu ameongeza kuwa kutokana na elimu inayotolewa mara kwa mara anamini wafanyabiashara wamehamasika na wako tayari kushiriki kukuza uchumi wa taifa kwa kuzingatia sheria.

MWISHO

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa