• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka Atoa Wito kwa Wadhamini Simiyu Jambo Festival kuendeleza Tamasha hilo

Posted on: July 1st, 2019

Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa Mkurugenzi wa Jambo Food Produsts Company, Mhe. Salum Khamis na wadhamini wengine waliojitokeza kudhamini Tamasha la Simiyu Jambo Festival kuliendeleza tamasha hilo kwa lengo la kuwasaidia wananchi wa mkoa wa Simiyu kuendeleza vipaji vyao katika sanaa, utamaduni na michezo.

Mtaka ameyasema hayo wakati akifunga Tamasha hilo Juni 30, 2019  Mjini Bariadi ambalo lilihusisha mashindano ya ngoma za asili (Mbina Wagika na Wagalu), mashindano ya baiskeli kwa wanawake na wanaume, mashindano ya mdahalo kwa wanafunzi wa shule za sekondari na mbio fupi(fun run).

“ Namshukuru sana Mkurugenzi wa Jambo Food Products Company Salum Khamis ambaye amekuwa mdhamini kwa miaka mitatu mfululizo kwenye tamasha  hili, nimuombe yeye na kampuni yake waendelee kuunga mkono juhudi hizi kwenye eneo la michezo na burudani, sisi ni viongozi leo tupo kesho hatupo, ni vizuri jambo hili ambalo tumelianzisha kampuni yake iendelee kulimiliki kama makampuni mengine ya vinywaji yanavyofanya” alisema ikaliendeleza.

Akizungumzia Kauli Mbiu ya Simiyu Jambo Festival: WEZESHA MTOTO WA KIKE ATIMIZE NDOTO ZAKE, INAWEZEKANA KUZUIA MIMBA KATIKA UMRI MDOGO; Mtaka amesema ni vema watoto wa kike walindwe ili waweze kuepuka mimba za utotoni na kufikia ndoto zao.

Akizungumza na wananchi wakati wa Tamasha la Simiyu Festival Mdhamini Mkuu wa Tamasha hilo Mkurugenzi wa Jambo Food Products Company Salum Khamis amesema Kampuni yake itaendelea kudhamni tukio hilo na kuahidi kuendeleza tamasha hilo.

Naye Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu Duniani(UNFPA) mkoani Simiyu, Dkt. Amir Batenga  amesema moja ya ahadi za shirika hilo ni kuwasaidia vijana kutimiza ndoto zao hivyo kupitia  kauli mbiu ya tamasha hilo shirika hilo lilifikisha ujumbe kwa vijana na wanaamini kila kijana anaweza kutimiza ndoto zake.

 Katika tamasha hilo washiriki zaidi ya 150 walishiriki mbio za baiskeli na mshindi wa kwanza  kilometa 150 wanaume alijinyakulia kitita cha shilingi 1,000,000/=, kilometa 80 wanawake shilingi 700,000 na walemavu kilometa tano shilingi 500,000/=, huku ngoma za asili Wagika na Wagalu kila kikundi kilijipatia shilingi 1,000,000/=

 Simiyu Jambo Festival mwaka 2019 imedhaminiwa na Jambo Food Products Company, Shirika la Umoja wa Mataifa Linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani-UNFPA, NGM Gold Mine Limited, NGS Petroleum, Alliance Ginneries Limited, Busega Mazao Limited, Maswa Standard Chalk, Ms Hotel,  Vetreces Company Limited na NHIF.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/07/rc-mtaka-atoa-wito-kwa-wadhamini-wa.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa