• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka atoa wito kwa KKKT kuendelea kuwekeza kwenye Miradi ya Maendeleo, Huduma za jamii Simiyu

Posted on: November 26th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameliomba Kanisa la Kiinjili na Kilutheri Tanzania (KKKT) kuendelea kuwekeza katika miradi ya maendeleo na huduma mbalimbali za jamii mkoani hapa.

Mtaka ameyasema hayo Novemba 25, wakati alipozungumza na waumini wa Kanisa hilo katika Usharika wa Tumain Bariadi Dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, ambapo alikuwa mgeni rasmi katika harambee ya ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa na matundu 10'ya vyoo katika Shule Awali na Msingi ya Tumaini (Tumaini Pre & Primary School) inayomilikiwa na kanisa hilo.

Amesema kanisa hilo limekuwa na mchango mkubwa katika miradi mingi ya maendeleo hususani katika sekta ya elimu, afya, maji na maeneo mengine muhimu ikiwemo sekta ya fedha ambapo Kanisa hilo linamiliki Benki ya Maendeleo.

"Pamoja na mradi huu wa shule ya msingi, tunaendelea kuliomba Kanisa kuona umuhimu wa kuwekeza katika miradi mingine ya maendeleo kwenye mkoa wetu; Kanisa lina hospitali, benki na vyuo vikuu; huu ni mkoa ambao bado haujawa na vyuo vikuu vingi kwa hiyo ipo nafasi kwa kanisa kuona kama linaweza kuwa na chuo cha ufundi, chuo cha kati au Tawi la Chuo Kikuu au kuwekeza katika eneo jingine ."alisema Mtaka.

Aidha, amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania kwa kuwa limekuwa sehemu ya mafanikio ya nchi yetu tangu imepata uhuru, kwani wapo Viongozi na Watanzania wengi katika maeneo tofauti nchini ambao wamepata elimu katika Vyuo na shule za kanisa, huku akisisitiza kanisa kuendelea kuombea amani na mshikamo wa nchi.

Naye Askofu wa KKKT, Dayosis ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria, Dkt. Emmanuel Makala amesema Kanisa litaendelea kushirikiana Serikali katika kuwafanya watu.wamjue Mungu na kuwaletea wananchi maendeleo, ambapo amebainisha kuwa ujenzi wa shule ni moja ya njia za kushirikiana na Serikali katika kuondoa ujinga na kujenga Taifa lenye watu walioelimika jambo ambalo litairahisisha Serikali katika kuwaongoza wananchi wake.

"Kanisa litaendelea kushirikiana na Serikali kuhakikisha watu wa Simiyu katika wilaya zote wanamjua Mungu; tunajenga shule ili tuondoe ujinga watu waelimike, ujinga ukiondoka hata Serikali inapata nafuu kuwaongoza watu wake" alisema Askofu Makala.

Awali akisoma risala kwa mgeni rasmi, Katibu wa Kamati ya Ujenzi, Mwl. Oberlin Kileo amesema ujenzi wa Shule ya Tumaini ulianza mwaka 2012, ambapo jumla ya vyumba vya madarasa tisa, matundu ya vyoo 10, jiko, stoo na viwanja vya michezo vilijengwa na kugharimu shilingi milioni 200 zikijumuisha na gharama za uwekaji wa miundombinu ya maji na umeme.

Ameongeza kuwa ili kujenga vyumba vya madarasa vitano na matundu 10 ya vyoo vivyokusudiwa kujengwa kwa awamu ya pili jumla ya shilingi milioni 120 zinahitajika.

Katika harambee hiyo jumla ya shilingi 41,526,500/= zilipatikana, kati ya hizo fedha taslimu zikiwa ni shilingi 7,466, 500 na ahadi shilingi 34, 060,000/= pamoja na vifaa mbalimbali vya ujenzi ikiwemo mifuko 60 ya saruji, nondo tani moja, mchanga lori kubwa nne na kokoto tripu mbili.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/11/rc-mtaka-atoa-wito-kwa-kkkt-kuendelea.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa