• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka Ataka Madiwani Itilima walipwe Madeni kabla ya Kumaliza Muda Wao

Posted on: July 3rd, 2019

Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameitaka Halmashauri ya wilaya ya Itilima kuhakikisha inawalipa madiwani wake malimbikizo ya madeni kupitia fedha za makusanyo ya pamba mwaka huu ili kuondoa usumbufu ambao unaweza kujitokeza pindi watakapokuwa wamemaliza muda wao.

Mtaka ameyasema hayo Julai 02, 2019 wakati akizungumza kwenye kikao cha Baraza maalumu la madiwani llililokuwa na agenda moja ya kujadili hoja 39 za ukaguzi zilizoibuliwa na mkaguzi na mthibiti mkuu wa hesabu za serikali ( CAG).

“ni vyema madeni ya waheshimiwa madiwani yakalipwa kwa wakati ni ngumu kujadili vitu vya kimaendeleo wakati wao wanadai, huwezi kushugulikia ya wengine wakati yako hayako vizuri,  ikumbukwe wamebakiza muda mfupi baraza livunjwe …si vyema wakatoka madarakani huku wakiwa wanadai”alisema Mtaka na kuongeza kuwa .

“Mkurugenzi hakikisha kipaumbele kwenye makusanyo ya pamba unalipa madeni ya waheshimiwa hawa (madiwani) hakikisha unahuisha bima zao, lakini kingine hakikisha unatenga fedha kwa ajili ya uchaguzi ” aliongeza.

Awali akisoma taarifa ya ripoti ya mkaguzi na mthibiti mkuu wa hesabu za serikali (CAG ) mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Elizabeth Gumbo alisema kwa mwaka wa fedha 2018/19 hoja zilizoibuliwa ni 39 na kuongeza kuwa hoja 24 kati ya 39 zilizoibuliwa zilitolewa mapendekezo na kuwasilishwa kwa mkaguzi na mthibiti mkuu wa hesabu za serikali kwa ajili ya uhakiki.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Mhe. Daudi Nyalamu amesema madiwani wanadai zaidi ya shilingi milioni 360 huku akiongeza tayari halmashauri imaishajipanga kulipa madeni yote kabla ya kuvunjwa kwa baraza hilo.

Nao baadhi ya madiwani akiwemo diwani wa kata ya Lugulu Robert Jongela na gertuda ngokolo diwani wa viti maalum kutoka kata ya ikindilo wamesema madeni yao ni ya muda mrefu tangu mwaka 2016 hadi 2019 hivyo kupitia kauli ya mkuu wa mkoa huo imewapa faraja na hatua hiyo imetoa tumain jipya la kupata stahiki zao,

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/07/rc-mtaka-ataka-madiwani-itilima-walipwe.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa