• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka Aongoza Harambee Ujenzi wa Bweni la Wasichana Mwanjolo Meatu, Zaidi ya Milioni 84 Zapatikana

Posted on: September 1st, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka ameongoza Harambee ya Ujenzi wa Bweni la Wasichana katika Shule ya Sekondari Mwanjolo Wilayani Meatu ambapo jumla shilingi milioni 84,876,950/= zimepatikana, fedha taslimu ikiwa shilingi 18,776,000/= ahadi 66,100,000/= pamoja na mifuko 253 ya saruji, mbuzi 12  na ng’ombe 3.

Akizungumza na wananchi na viongozi wa Chama na Serikali Mtaka amewapongeza viongozi wa kata ya Mwanjolo kwa jitihada walizofanya kwa kushirikiana na wananchi katika kuhakikisha wanafunzi wa kike wanapata bweni, huku akiwasisitiza wananchi kuona umuhimu wa kuwekeza katika elimu ili kuuweka mkoa huo kwenye ushindani na mikoa mingine.

Aidha, ametoa wito kwa Madiwani wa kata zote mkoani humo kuiga mfano wa Kata ya Mwanjolo ambapo amesema viongozi na wananchi wanapaswa kuona uchungu na kuona haja ya kuwa na mabweni kwa watoto wa kike ili waondakane na vishawishi na changamoto nyingine zinazowakabili ili waweze kufikia malengo yao.

“Madiwani wetu hili jambo waige, haiwezekani hawa wasichana wadogo wanaenda kupanga kwenye vijiji pateni uchungu watoto wa kike wajengewe hosteli, Mungu ametupa ardhi, mifugo, nguvu za kufanya kazi, tukishikamana kama watu wa Mwanjolo, watoto wetu wa kike wote watapata mabweni”

“Mwanjolo wametuamasha, niwaombe waheshimiwa madiwani na viongozi wenzangu kwenye wilaya zote za Mkoa wa Simiyu moto huu uliowashwa hapa Mwanjolo uende kwenye kata zote, tuanze kujenga mabweni ya watoto wa kike wanapofaulu kwenda kidato cha kwanza wakae shule wasitembee njiani wakaanza kupewa lift za baiskeli na bodaboda” alisema Mtaka

Ameongeza kuwa kwa sababu elimu ni kipaumbe cha kwanza cha mkoa ni vema viongozi wote mkoani humo wakaweka dhamira kuwa kufikia mwaka 2020 wanafunzi wa kike wote wanaosoma shule za sekondari mkoani Simiyu wakae bweni.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kisesa wilayani Meatu Mhe. Luhaga Mpina ametoa wito kwa Wananchi hususani jamii ya wafugaji kuchangia na kuunga mkono jitihada mbalimbali za maendeleo ya elimu ili watoto wa jamii za kifugaji waweze kusoma katika mazingira mazuri.

Wakati huo huo amewahimiza vijana wanaotoka katika jamii za kifugaji kusoma kwa bidii ili waweze kuzisaidia jamii zao kufuga ufugaji wenye tija utakaowaletea manufaa.

Nao wanafunzi wa kike wa Shule ya Sekondari Mwanjolo wamewashukuru viongozi na wananchi ambao wamechangia ujenzi wa bweni, ambapo wamesema endapo bweni hilo litakamilika litawasaidia kuondokana na vishawishi mbalimbali vilivyokuwa vikisababisha baadhi yao kupata ujauzito na kushindwa kumaliza masomo yao.

“Kukamilika kwa bweni kutatusaidia kutatua changamoto tunazokutana nazo sisi wasichana hasa suala la mimba, kuna wenzangu nilioanza nao kidato cha kwanza mwaka 2016 hawapo shuleni sasa hivi sababu ya mimba, naamini tukikaa bweni tutakuwa salama  na tutapata muda mwingi wa kujisomea kwa kuwa hatutatembea mwendo mrefu tena”  Eunice Kapombe mwanafunzi Kidato cha Tatu.

Kwa upande wao wazazi na walezi wa baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mwanjolo wamesema ujenzi wa bweni la wasichana katika Shule ya Sekondari Mwanjolo utakuwa msaada mkubwa kwa watoto wa kike katika kuwawezesha kufikia kwenye malengo yao,kwa kuwa baadhi yao wamekuwa wakikatisha masomo kutokana na mimba zinazosababishwa na vishwawishi wanavyopata kwa kutembea mwendo mrefu kwenda shule na baadhi yao kupanga vijijini.

Harambee ya ujenzi wa Bweni la Wasichana Shule ya Sekondari Mwanjolo iliyofanyika Shuleni hapo Agosti 31, 2018,  imehusisha viongozi wa Chama na Serikali ngazi ya Mkoa na Wilaya ya Meatu, Wadau mbalimbali wa Maendeleo na wananchi, ambapo mpaka kukamilika kwa Bweni hilo jumla ya shilingi 125,024,504.35 zitahitajika.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/09/rc-mtaka-aongoza-harambee-ujenzi-wa.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa