• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka aahidi kuleta Mapinduzi ya Michezo, Simiyu kuendesha Michezo Kibiashara

Posted on: December 17th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amezindua mashindano ya taifa ya mpira wa kikapu na kusema kuwa Simiyu imedhamiria kuleta mapinduzi katika sekta ya michezo kama njia kukuza vipaji na kuongeza ajira kwa vijana.

Akizindua mashindano hayo yanayofanyika kwa mara ya kwanza katika uwanja wa halmashauri ya mji wa bariadi, Mhe Mtaka amesema mashindano hayo ni kielelezo cha jitihada za mkoa wa Simiyu katika kuhakikisha unatumia michezo kama biashara na kuondokana na utamaduni wa kutumia michezo kujiburudisha.

Mtaka ameongeza kuwa mashindano haya yatatumika kama darasa litakalo uwezesha mkoa kujipanga vizuri na kuandaa timu zake kwa mashindano yajayo huku akisisitiza kuwa mkoa wa Simiyu utaendelea kuibua fursa mbalimbali kupitia michezo kama njia kukuza uchumi na kuimarisha mahusiano ya kijamii.

“Bila shaka nyote mmejionea jinsi tulivyo wekeza kwa gharama kubwa, tumetengeneza uwanja huu wenye ubora wa kipekee nchini, naomba niwahakikishie tutautumia kikamilifu kuleta mapinduzi ya mchezo wa mpira wa kikapu mkoani kwetu hasa kwa kuibua vipaji vipya, pia tutatumia mashindano ya UMISHUMTA na UMISETA kupata timu bora ambayo ninaamini ndio watakuwa mabingwa wa baadae wa mchezo huu, alisisitiza Mtaka”.

Adha Mhe Mtaka amemwagiza afisa elimu wa mkoa kuandaa mpango wa kuboresha mchezo huo ikiwa ni pamoja na kuwabaini na kuwatumia walimu wenye uwezo wa kufundisha mpira wa kikapu ili waweze kuziandaa timu za mkoa kwa mashindano mbalimbali.

Kwa upande wake Makamu wa rais wa shirikisho la mpira wa kikapu nchini Mboka Mwambusi amesema kutokana na mchango mkubwa wa mkuu wa mkoa wa Simiyu katika kufanikisha mashindano hayo, shirikisho hilo limeamua kuyaita mashindano ya taifa ya mpira wa kikapu ya Mtaka.

“Sote ni mashuhuda wa jitihada za mheshimiwa Anthony Mtaka katika kufanikisha mashindano haya, mtakumbuka tulihangaika sana kutafuta mkoa utakaoratibu shughuli hii, ni Simiyu pekee ndio walikubali kwa moyo mkunjufu, hivyo tumeona zawadi pekee ni kuyapa jina la aliyefanikisha zoezi hili, aliongeza Mwambusi”.

Naye Katibu wa Shirikisho la mpira wa kikapu nchini Bakari Ramadhani amesema mashindano hayo yatatumika kama chachu ya kuibua vipaji vipya halikadhalika yatatumika kuwapata wachezaji bora watakaounda timu ya taifa ya mpira wa kikapu kwa siku za baaadae.

Mashindano hayo yanayoshirikisha timu kutoka mikoa 8 yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 22 Disemba ambapo mshindi atakabidhiwa kikombe.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa