• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RAS Simiyu Azindua Utafiti wa Matumizi ya Simu Katika Kuongeza Ulipaji Kodi za Majengo

Posted on: November 29th, 2019

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amezindua rasmi utafiti unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 ambao utafanyika kuanzia Novemba 28, 2019 hadi 30 Juni 2020 katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi na Halmashauri ya Wilaya ya Busega.

Akizindua utafiti huo Novemba 28, 2019 mjini Bariadi Sagini amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri hizo kutoa ushirikiano unaotakiwa kwa watafiti ili kuwawezesha kufanya kazi yao kwa ufanisi na kupata matokeo sahihi.

 

 “ Wakurugenzi katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi na Busega, hakikisheni mnatoa ushirikiano katika utafiti kwani majengo yanayolipiwa kodi ya majengo yapo kwenye maeneo yenu na wamiliki wa majengo hayo pia wapo katika maeneo yenu,” alisema Sagini.

Sagini amewaahidi watafiti ushirikiano mkubwa ili utafiti ufanyike kama ilivyokusudiwa kwa lengo la kuongeza mapato yatokanayo na kodi ya majengo huku akiwaomba watafiti hao  kuendeleza kushirikiano na mkoa wa Simiyu katika tafiti mbalimbali kwa maendeleo ya Mkoa, wananchi na Taifa kwa ujumla.

Akiwasilisha taarifa ya utambulisho wa utafiti huo Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Mzumbe na Mtafiti Mwandamizi wa Utafiti huu, Dkt.Francis Mwaijande, amesema Matokeo ya utafiti huu yatawezesha mamlaka za maamuzi ziweze kutoa maamuzi kwa kuzingatia taarifa zilizifanyiwa utafiti na hivyo kuwa na maamuzi ya kuongeza ufanisi kwenye ukusanyaji kodi.

Ameongeza kuwa matokeo ya utafiti huu yanatarajiwa kuongeza mapato yatokanayo na kodi za majengo kwa Serikali kwa kuhamasisha ulipaji kodi kwa kutumia simu zao za mkononi kwa njia ya meseji.

Utafiti unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 unafanyika kwa lengo la kutafuta Ushahidi wa kitaaluma ili kuainisha kipi kinaweza kuongeza ulipaji kodi kwa kufuata sheria.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/11/ras-simiyu-azindua-utafiti-wa-matumizi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa