• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RAS Simiyu awataka Watumishi Simiyu kuwa Mabalozi wa Maadili ya Utumishi wa Umma

Posted on: March 15th, 2019

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amewataka watumishi wa Umma mkoani humo kuwa mabalozi wema wa maadili ya utumishi wa umma katika maeneo ya kazi ikiwa ni pamoja na kutopokea zawadi kwa wananchi wanaowahudumia kwa kuwa wanalipwa mshahara na Serikali kwa kazi hizo.

Sagini ameyasema hayo Machi 14, 2019 Mjini Bariadi wakati akifungua mafunzo ya Kamati za Kudhibiti Uadilifu za Mkoa wa Simiyu, yanayoendeshwa na Mratibu wa Utawala Bora kutoka Ofisi ya Rais kwa kushirikiana na Maafisa kutoka TAKUKURU na Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Amesema watumishi wa umma wanalipwa mishahara ili waweze kuwahudumia wananchi hivyo hawapaswi kudai chochote kutoka kwa wananchi.

"'Acheni kupokea vizawadi vidogo vidogo kwa huduma tunazotoa kwa wananchi ambazo tunalipwa mshahara kutokana na huduma hizo; muwe mabalozi wa kueneza maadili mema kwa watumishi wenzenu na nje ya maeneo yenu ya kazi ili ofisi zetu za Umma mkoani Simiyu ziwe mfano wa kuigwa" alisema Sagini.

Aidha, Sagini amezitaka kamati zote za kudhibiti uadilifu mkoani Simiyu mara baada ya mafunzo ziandae mpango kazi wa namna ya kushughulikia kero mbalimbali za watumishi zinazohusiana na ukiukwaji wa maadili katika utumishi wa Umma, ili kuwa na watumishi wanaozingatia sheria, kanuni na miongozo mbalimbali ya Utumishi wa Umma.

Akitoa taarifa ya mwenendo wa makosa ya rushwa kwa watumishi wa umma, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Simiyu, Bw. Adili Elinipenda ametoa wito kwa Wakurugenzi kutoa ushirikiano kwa TAKUKURU kuona namna watakavyosaidia pale wanapoletewa barua za kuwafikisha watumishi mahakamani  kwa makosa ya rushwa ili kutokuharibu ushahidi.

“Kesi tulizonazo mahakamani nyingi ni za watumishi wa umma na baadhi ya mashahidi tunaowahitaji wanatoka ofisi hizo hizo sasa wakurugenzi wamekuwa hawawasimamishi kazi,  kwa hiyo imekuwa ngumu kwa mtumishi kumtolea ushahidi mtumishi mwenzake aliye naye ofisi moja na wakati mwingine ni bosi wake, sasa hapa nafikiri mtaona ni busara gani itumike tunapowatumia barua za kuwafikisha watu mahakamani” alisema Mkuu huyo wa TAKUKURU.

Naye Mratibu wa Utawala Bora kutoka Ofisi ya Rais Ikulu, Bw. Apolinari Tamayamali amesema ni vema Mamlaka za Serikali za Mitaa zikazingatia utaratibu wa sheria unaopaswa kufuatwa wakati mtumishi anapohukumiwa kifungo au faini ili kupata ufumbuzi wa suala hilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Utumishi na Utawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, Bi. Pendo Haule kuhusu kusimamishwa kazi kwa mtumishi ambaye ameshtakiwa mahakamani amesema kwa mujibu wa Kanuni za Utumishi wa Umma za mwaka 2003, sheria imempa nafasi  mwajiri ya kumsimamisha kazi au kutomsimamisha kazi mtumishi  ambaye ana kesi mahakamani, lakini ikiwa kuwepo kwa mtumishi huyo kazini kunaweza kuharibu ushahidi ni vema sheria ikafuatwa akasimamishwa kazi.

Awali akizungumzia  lengo la kuandaa mafunzo kwa kamati za kudhibiti wa Uadilifu,  Mratibu wa Utawala Bora kutoka Ofisi ya Rais Ikulu, Bw. Apolinari Tamayamali, amesema ni kuwezesha kamati hizo kupata uelewa wa pamoja juu ya mkakati wa mapambano dhidi ya rushwa awamu ya tatu, namna ya kuandaa mpango kazi na utoaji wa taarifa katika masuala ya mapambano dhidi ya rushwa hapa nchini.

Ameongeza kuwa jithada hizi za kutoa elimu kwa kamati za udhibiti wa uadilifu zimaeanza mwaka 2017, ambapo hadi kufikia mwaka 2018 mikoa takribani 16 imefikiwa na kwa sasa timu ya wataalam iko katika mikoa yote 10 iliyo salia ili kukamilisha mikoa yote 26 ya Tanzania Bara.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGU KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/03/ras-simiyu-awataka-watumishi-simiyu.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa