• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RAS Simiyu Ataka Majengo ya Upasuaji, Wodi Ya Wazazi Hospitali ya Wilaya Busega Yakamilishwe

Posted on: September 9th, 2020

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Bw. Anderson Njiginya kutoa fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa majengo ya upasuaji na wodi ya wazazi katika Hospitali ya Wilaya ili kuboresha hali ya utoaji wa huduma kwa wananchi katika hospitali hiyo. 

Mmbaga ametoa agizo hilo Septemba 09, 2020 wakati zoezi la usimamizi shirikishi alipotembelea hospitali hiyo kukagua maendeleo ya ujenzi wa majengo hayo ambayo yanapaswa kukamilika na kuanza kutoa huduma ifikapo Septemba 30, 2020.

“Nampongeza Mkurugenzi kwa kujiongeza, badala ya kusubiri kibali kutoka HAZINA kulipa fedha za kukamilisha ujenzi wa majengo haya, amejiwekea utaratibu wa kuwalipa mafundi wetu, nimeelekeza kuwa aongeze kiwango anachotoa kwa kila juma ili kuongeza kasi ya ujenzi na hatimaye majengo haya yaweze kukamilika na kutumika kwa huduma kusudiwa,” alisema Mmbaga.

Aidha, Mmbaga ameongeza kuwa ukamilishaji wa majengo hayo uende sambamba na utunzaji wa mazingira ambao utajumuisha upandaji miti, bustani za maua na utunzaji wa miti asili huku akitoa pongezi kwa Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri hya Wilaya ya Busega kwa usimamizi mzuri katika ujenzi wa hospitali hiyo na kumuagiza Mkurugenzi kumthibitisha katika cheo chake.

Wakati huo huo Mmbaga ameelekeza Timu ya usimamizi wa afya ngazi ya wilaya (CHMT) kuimarisha usimamizi katika mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) uliboreshwa hususani watoa huduma ngazi ya jamii wanaohusika katika usajili ili wananchi waweze kupata huduma zilizokusudiwa  na serikali.

Katika hatua nyingine Mmbaga ametembelea kikundi kinachojihusisha kilimo cha umwagiliagi kilichopo kijiji cha Chamgasa na kuelekeza wataalam wa fedha na uchumi waweze kutoa elimu kwa wakulima hao juu ya utunzaji na matumizi ya fedha ili wanapopewa mikopo na wadau waweze kutekeleza miradi ambayo itakuwa endelevu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Bw. Anderson Njiginya amesema atahakikisha fedha zinatolewa kwa wakati kwa mafundi wanaoendelea na ujenzi wa majengo ya Upasuaji na wodi ya wazazi katika hospitali ya wilaya ili shughuli za ujenzi zisikwame.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba ameipongeza Timu ya usimamizi wa afya ngazi ya wilaya (CHMT) kwa namna inavyotekeleza majukumu yake huku akisisitiza watumishi wote wa afya kuendelea kutoa huduma stahiki  kwa wananchi.

Nao baadhi ya watumishi wa afya katika kituo cha afya Lukungu wameomba miundombinu katika vituo vya kutolea huduma za afya iboreshwe ili kutoa huduma kulingana na hadhi za vituo hivyo na wananchi wapate huduma wanazotarajia kuzipata katika vituo husika.

MWISHO.

KUPATA PICHA ZAIDI TAFADHALI TEMBELEA BLOGU YETU YA MKOA KUPITIA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/09/ras-simiyu-ataka-majengo-ya-upasuaji.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa