• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Pinda Afungua Kongamano La Kilimo Biashara Nanenane Simiyu

Posted on: August 6th, 2019

Waziri Mkuu Mstaafu wa Awamu ya nne, Mhe. Mizengo Pinda, amefungua Kongamano la Kilimo Biashara katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayoendelea katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu, ambapo amesema kilimo biashara kinaweza kutoa mwongozo wa changamoto ya tija ndogo katika kilimo; ikiwa ni pamoja na matumizi ya kilimo cha umwagiliaji, matumizi ya teknolojia sahihi katika uzalishaji na hifadhi ya mazao.

Mhe. Pinda ameyasema hayo Agosti 06, 2019  mjini Bariadi katika kongamano la Kilimo Biashara lililofanyika wakati wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayofanyika Kitaifa Kanda ya Ziwa Mashariki Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu.

Mhe. Pinda amesema kuwa ni vyema wakatumia teknolojia za kisasa zilizopo  ili waweze kupata tija kwenye kilimo ambacho kina mchango katika pato la Taifa na kubainisha kuwa mchango wake bado ni mdogo kutokana na sababu nyingi ikiwemo mabadiliko ya hali ya hewa hatua inayopelekea kilimo kutokuwa na tija ya kutosha.Ameongeza kuwa hakuna haja kwa wakulima kulima kwa kutegemea mvua ilihali maeneo  mengi ya Mikoa ya Kanda ya Ziwa yanazungukwa na ZiwaVictoria  lenye maji mengi ambayo yakitumika vizuri wataweza kuzalisha mavuno mengi kwenye eneo dogo kupitia umwagiliaji na teknolojia za kisasa zilizopo.

“niishauri tu Mikoa hii ambayo inazungukwa na Ziwa lenye maji mengi ambayo nchi jirani zinatumia maji hayo kuzalisha mazao kutokana na umwagiliaji badala ya kutegemea mvua; unapotokea ukame unaathiri mazao hayo ipo haja ya kuona umuhimu wa kwenda  kwenye kilimo cha umwagiliaji”alisema waziri mkuu mstaafu PindaKwa upande wake Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga amesema sekta ya kilimo ina uwezo wa kuongeza pato la Taifa kwani inachangia kwa asilimia 28.7 huku akibainisha kuwa tija ya uzalishaji kwa wakulima bado ipo chini huku akikisitiza matumizi sahihi ya ardhi na maji hususani kwenye shughuli za umwagiliaji.Ameongeza kuwa licha ya asilimia 65.5 ya Watanzania kujiajiri kwenye sekta ya kilimo moja kwa moja asilimia 66% zinahitajika kwenye viwanda na kwamba zinatakiwa kuboreshwa ili ziweze kufikia angalau 80%.

Katika hatua nyingine Mhe. Hasunga ametoa wito kwa wawekezaji  kuwekeza kwenye viwanda vya mafuta kwani Serikali inatumia fedha nyingi kuagiza mafuta nje ya nchi licha ya kuwa mazao mengi yana malighafi ambazo zina uwezo wa kutengeneza mafuta ya kula zipo nchini.“tuna mazao mengi ambayo malighafi zake zina uwezo wa kutengeza mafuta lakini serikali inatumia fedha nyingi kuagiza nje ambapo kwa mwaka ni tani 570,000 huku uwezo wa kuzalisha ukiwa ni tani 250,000 na katika hili tutatumia maamuzi magumu ili tuwekeze kwenye viwanda vya mafuta” alisema waziri Hasunga.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka ameyataka  makundi ya wanawake, vijana  na waoneshaji kwa ujumla wake kutumia fursa ya uwepo wa Kongamano la Kilimo Biashra kujifunza ili waweze kuongeza ujuzi ambao utaenda sambamba na kutambua mnyororo wa thamani kwenye mazao na shughuli zao za kilimo.

Hata hivyo  Mkurugezi wa Mtendaji Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF) Tausi Kida amesema kuwa wakati umefika kwa wakulima kutumia maeneo madogo kuzalisha uzalishaji wenye tija unaoenda sambamba na mazao bora ambayo yatakuwa na uhakika kwenye masoko ya nje.

MWISHO.

kUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/08/waziri-mkuu-mstaafu-pinda-afungua.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa