• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

NBC Yaahidi Kufungua Tawi Mjini Bariadi Simiyu

Posted on: August 7th, 2018

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Taifa ya Biashara(NBC) ,Theobald Sabi amewahakikishia wakazi wa Bariadi Mkoani Simiyu kuwa Benki hiyo itafungua tawi Mjini Bariadi ili kusogeza huduma karibu na wananchi.

Sabi ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Wakala Mkubwa (Super Agent) Mjini Bariadi, Agosti 07, 2018.

Amasema Wilaya ya Bariadi na Mkoa wa Simiyu ina wateja wengi wa NBC lakini huduma zilikuwa mbali hivyo, kufunguliwa kwa wakala mkubwa (SUPER AGENT) ni sehemu ya mpango wa kupeleka karibu huduma kwa wateja wao.

“Hapa Bariadi tuna wateja wengi lakini huduma zilikuwa zinapatikana mbali, hivyo kufunguliwa kwa wakala huu ni kutawasaidia wateja wetu kupata huduma karibu na tutaendelea kuongea na wananchi ili tuweze kupata tawi la NBC,  ni nia yetu hivi karibuni kuongeza tawi hapa Bariadi” alisema .

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema kufunguliwa kwa Wakala Mkubwa wa NBC Bariadi kumekuja katika wakati muafaka ambapo utaweza kupima mzunguko wa fedha mjini Bariadi na kuwa njia ya kwenda kwenye kufungua Tawi kamili la NBC.

Amesema Mkoa wa Simiyu ni mkoa mpya unaojengwa kiuchumi hivyo ikiwa benki hiyo ikijipanga vizuri Wakala huo uliofunguliwa utafanya biashara kwa kuwa wakazi wa mkoa wa Simiyu ni wafayabiashara wazuri wa mazao mbalimbali pamoja na mifugo.

“Mkoa wa Simiyu ni mkoa wenye Uchumi mzuri tunao uwezo wa kuzungusha zaidi ya Bilioni 100 wakati wa mavuno ya pamba, benki ikijipanga vizuri na ikapata msimamizi mzuri wa wakala anayefahamu biashara ya benki mtafanya biashara, Wanyantuzu ni wafanyabiashara hakuna Mnyantuzu mcheza pulu” alisema

Naye Mfanyabiashara wa Mjini Bariadi, Bw. John Sabo ameshukuru uanzishwaji wa  Wakala huo  ambao utawapunguzia adha ya kufuata huduma mikoa ya Mwanza na Shinyanga  na kuabainisha kuwa  Wakala tu hautoshi, hivyo wafanyabiashara wengi wenye akaunti NBC wanaomba Benki ya NBC kufungua Tawi kamili Mkoani Simiyu.

MWISHO.

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/08/benki-ya-nbc-yaahidi-kufungua-tawi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa