• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Naibu Waziri Mgumba Aagiza Tume ya Umwagiliaji kufanya Tathmini Ujenzi wa Bwawa Skimu ya Umwagiliaji Maswa

Posted on: March 8th, 2019

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba amemuagiza Mhandisi wa Umwagiliaji Tume ya Umwagiliaji Kanda ya Mwanza, Ebenezer Kombe kufanya tathmini katika Skimu ya Umwagiliaji ya Kinamwigulu Wilayani Maswa, kuona kama kuna uwezekano wa kujenga bwawa, ili Serikali iweke mipango ya kujenga bwawa hilo kuwawezesha wananchi kulima bila kutegemea mvua.

Mhe. Mgumba ameyasema hayo wakati alipotembelea eneo la skimu hiyo na kupokea ombi kutoka kwa wananchi la kuomba kujengewa bwawa na kuboreshewa mundombinu mingine, wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua shughuli za kilimo na miradi ya umwagiliaji wilayani Maswa Machi 07, 2019.

Amesema mara baada ya kupokea taarifa ya tathmini itakayofanywa na wataalam wa umwagiliaji ikionekana katika eneo hilo Bwawa linaweza kujengwa Serikali itahakikisha inaweka  katika Mpango wa bajeti fedha kwa ajili ya bwawa hilo, ili kukidhi haja ya wananchi ya kulima kwa umwagilia kwa lengo la kujikwamua kiuchumi.

“Mhandisi wa Umwagiliaji wa Kanda ni vizuri ukaja hapa na wataalam mkafanya tathmini kuona je inawezekana kujenga mabwawa hapa, baada ya tathmini tukishafahamu kuwa panafaa kujenga bwawa ndiyo tuweke katika mpango wa bajeti” alisema Mgumba.

Kwa uapnde wao Wananchi hao wamesema wakijengewa bwawa na kuboreshewa miundobinu umwagiliaji watakuwa na uhakika wa kulima bila kutegemea mvua angalau mara mbili kwa mwaka, ambapo pia wameomba kuwezeshwa zana bora za kilimo.

“Tunaiomba Serikali itujengee bwawa kuendeleza kilimo cha umwagiliaji ili  kusudi tuwe tunalima mara mbili kwa mwaka badala ya kutegemea mvua peke yake” alisema mkulima wa Kinamwigulu

“Pamoja na ombi la kutujengea bwawa litakalotusaidia kulima misimu miwili kwa mwaka tunaomba pia Serikali ituletee mikopo ya matrekta ili tuweze kulima maeneo makubwa zaidi” alisema Charles Hege mkulima wa Kinamwigulu

Katika hatua nyingine Mhe. mgumba amesisitiza suala la Halmashauri kutenga asilimia 20 ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kuendeleza shughuli za uzalishaji ikiwemo kilimo kwa kuwa zina mchango mkubwa katika mapato ya Halmashauri, badala ya kuwekeza fedha nyingi kwenye miradi ya kutoa huduma pekee.

Awali akitoa taarifa ya Wilaya, Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe ameiomba Bodi ya Pamba kuwashirikisha viongozi wa Wilaya na Halmashauri katika kuandaa mwongozo wa ununuzi wa pamba, ili waweze kupata nafasi ya kutoa maoni yao kwa kuwa ni wadau muhimu na wasimamizi wakubwa katika uzalishaji wa zao hilo.

Akiwa Wilayani Maswa, Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba ametembelea skimu ya umwagiliaji ya Kinamwigulu na shamba la pamba lenye ukubwa wa ekari tano linalomikiliwa na kikundi cha wanawake kiitwacho Upendo, kilichopo Kijiji cha Busamda.

MWISHO

 KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/03/naibu-waziri-mgumba-aagiza-tume-ya.html


Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa