• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Naibu Waziri Mavunde awataka Kidato cha Sita Simiyu wasikubali Ndoto zao Kukatishwa

Posted on: April 20th, 2019

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana na Ajira, Mhe.Anthony Mavunde ametoa wito kwa wanafunzi wa kidato cha sita Mkoani Simiyu kutokubali mtu yeyote kufifisha wala kukatisha ndoto zao badala yake wasome kwa bidii.

Mavunde ametoa wito huo wakati akizungumza na wanafunzi zaidi ya 1000 kutoka  shule kumi na mbili za sekondari za kidato cha sita walioko katika kambi ya kitaaluma, shule ya sekondari ya wasichana Maswa.

Mavunde amesema Taifa lolote duniani linajengwa na vijana na hasa vijana wasomi hivyo wanapaswa kusoma kwa bidii, ili wasiwaangushe, wazazi na jamii inayowazunguka  ambayo inawategemea, huku akipongeza uongozi wa mkoa kuanzisha kambi za kitaaluma ambazo zimeoneka kuusaidia mkoa kupanda katika ufaulu.

“wanafunzi msikubali ndoto zenu zikatishwe, someni kwa bidii mfikie ndoto zenu, Taifa wazazi na jamii inayowazunguka inawategemea, msiwaangushe viongozi wenu waliofanya mkawa hapa, Mkoa wa Simiyu ndio umetuonesha kuwa kumbe kambi za kitaaluma zinawezekana” alisema Mhe. Mavunde.

Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewapongeza walimu wote kwa kazi nzuri wanayoifanya  na kueleza  lengo la kuanzishwa kambi za kitaaluma ambazo amesema zimeonekana kuwa na mwamko mkubwa kwa wanafunzi.

“Sisi tulitafakari watoto wetu wanatoka kwenye mazingira ya kawaida tukajiuliza kwa nini wasikae kwenye madarasa yaliyo na sakafu na dari safi wakasoma, tumejaribu kwenye shule za O’level (kidato cha nne) tumeona mwamko wa watoto kusoma” alisema Mhe. Mtaka.

Kwa upande wao viongozi na wadau mbalimbali wa elimu waliowatembelea wanafunzi hao pia walipata nafasi ya kuwausia wanafunzi hao wa kidato cha sita na kuwasisitiza juu ya umuhimu wa kufanya bidii ili kufikia malengo  yao.

“ Tunajadiliana hapa ili kuwa na uelewa wa pamoja, ninataka kuwaambia kuwa hakuna mafanikio yanayokuja kwa bahati mbaya iwe  katika masomo hata katika maisha,” alisema Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisha.

“Mnaweza kutimiza ndoto zenu bila kujali mahali mtu anapotoka, najua wengi wetu hapa tumetoka katika familia za kawaida, tumesoma shule za kawaida kabisa lakini tulifanikiwa, hata ninyi mnaweza ni suala la kuamua tu” alisema Happiness Lugiko Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki.

Naye Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo Kuu la kusini, Mch. Mark Malekana amesema ili wanafuzi hao waweze kufikia ndoto zao wanapaswa kuwa na dhamira ya kushinda, wasome kwa bidii, wawe na nidhamu, washinde hofu wanapokuwa kwenye mitihani na wamwamini Mungu.

Mwanafunzi Kelista Joseph kutoka shule ya sekondari Itilima amesema maswali mbalimbali ambayo wamekuwa wakiyafanyia kazi yatawasaidiana mwishowe watafanya vizuri  na wanaamini kama walivyoahidi toka siku ya kwanza ya kambi kwamba watapata ‘Division One’ wote.

Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019 Mkoani Simiyu inatarajiwa kufungwa rasmi Aprili 28, 2019 na baadaye wanafunzi watarejea katika shule zao kwa ajili ya maandalizi ya Mtihani wa Taifa unaotarajia kuanza Mei 06, 2019.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII  FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:https://simiyuregion.blogspot.com/2019/04/naibu-waziri-mavunde-awataka-kidato-cha.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa