• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Naibu Waziri Madini atoa Siku Moja kwa Makandarasi Kukamilisha Jengo la Soko la Madini Simiyu

Posted on: May 3rd, 2019

Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Stanslaus Nyongo ametoa muda wa siku moja kwa Mkandarasi  SUMA JKT anayejenga Jengo la Kituo cha Umahiri Simiyu kuamilisha sehemu ya Jengo hilo iliyopangwa kutumika kama Soko la Madini la Mkoa.

Nyongo ameyasema hayo Mei  02, 2019 wakati alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo ambalo sehemu litatumika kama kituo cha umahiri na sehemu kama Soko la Madini la Mkoa.

“ Kwa  mkoa wa Simiyu tumeona hapa tunaweza kupatumia kwa kuanzia kwenye soko la madini, nimeshatoa maagizo kuwa jengo hili walimalizie mara moja, ili waweze kutoa sehemu ambayo itatumika kwa ajili ya soko la madini na kufikia kesho jioni tunataka jengo hili lianze kutumika kama soko la Madini “ amesema Nyongo.

Aidha, Nyongo amesema anatumia  fursa hiyo kuwajulisha wachimbaji  wadogo wadogo wa madini kuwa Simiyu kutakuwa na jengo ambalo litatumika kununua na kuuza madini.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema kama mkoa wamejipanga vizuri katika soko la madini, huku akiwakaribisha wafanyabiashara wa madini kutoka mkoa wa Simiyu  na mikoa jirani kufika katika kituo hicho ambacho amesema kitakuwa kituo bora chenye uhakika wa kufanya biashara hapa nchini.

Mtaka ameongeza kuwa kituo hicho ambacho kitafunguliwa rasmi wiki ijayo kitatoa fursa kwa Watanzania kuanza kuangalia ufanyaji wa biashara katika eneo la madini kwa njia ambazo ni halali, akatoa wito kwa wafanyabiashara wa mkoa wa Simiyu pamoja na kuwekeza biashara katika kilimo, mifugo na viwanda wawekeze pia katika biashara ya madini.

Naye Sajenti Emmanuel Igogo kutoka SUMA JKT amesema agizo la Naibu Waziri la kukamilisha sehemu ya Jengo la Kituo ca Umahiri ambayo itatumika kama soko la madini (Kituo cha kuuzia madini) litatekelezwa kama lilivyoagizwa.

“ Tutatekeleza agizo la Mhe. Naibu Waziri tutaanza leo kulifanyika kazi na kwa kuwa kazi hii haikuwepo kwenye mkataba wetu wa awali nitawasiliana na viongozi wangu na tutakamilisha” alisema Sajenti Igogo.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/05/naibu-waziri-madini-atoa-siku-moja-kwa.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa