• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Naibu Waziri Mabula ashauri Wizara ya viwanda kuanzisha kliniki za Biashara ngazi ya Kanda Kuwasaidia Wafanyabiashara

Posted on: October 27th, 2018

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula ameshauri Wizara ya Viwand, Biashara na Uwekezaji kuona namna ya kuwa na Kliniki za Biashara ngazi ya kanda ili kuwasaidia wafanyabiashara hususani wale wanaoanza, wajasiriamali wadogo na wasiojua taratibu za uendeshaji wa biashara zao kujua na kuwa wafanyabiashara wazuri.

Mhe.Mabula ameyasema hayo mara baada ya kutembelea banda la Maonesho la Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara(TanTrade) katika Maonesho ya Viwanda Vidogo (SIDO) yanayoendelea katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.

Amesema amepongeza Wizara ya Viwanda, Biashara na uwekezaji kubuni Kliniki ya biashara ambayo inachangia kuwandaa wafanyabiashara kufahamu wafanye nini kabla na baada ya kuanzisha biashara na kufanya biashara zao kwa kuzingata sheria, kanuni na taratibu za nchi hii

“Ili mtu awe huru kufanya biashara yake ni lazima zingatie sheria kanuni na taratibu za nchi hii, mtu anapokuja kwenye kliniki hii anaambiwa kabla ya kuanza anatakiwa apitie hatua zipi na aweke mazingira yapi, ili atambulike na TRA anapaswa afanye nini  na mambo mengine mengi na wakizingatia wanachoambiwa hapa hawahitaji kukimbizana na mgambo wa polisi”

“Ninashauri Wizara ya Viwanda ione namna ya kuwa na kliniki za biashara kikanda ili wafanyabiashara wanaoanza, wajasiriamali wadogo na wale wasiojua taratibu waweze kujua taratibu na wawe wafanyabiashara wazuri” alisema Mhe. Mabula.

Afisa Biashara Mwandamizi kutoka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara hapa nchini (TanTrade) Bi. Magdalena Shirima amesema hadi kufikia Oktoba 26, 2018 wajasiriamali zaidi ya 60 walioshiriki katika Maonesho ya SIDO Kitaifa wamehudhuria Kliniki hiyo kupata huduma.

Baadhi ya Wajasiriamali waliopata nafasi ya kushiriki na kupata huduma za ushauri wa kibiashara kupitia Kliniki hiyo wamesema imewasaidia kubadili mitazamo dhidi ya biashara zao na kufahamu mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na uanzishaji wa biashara, namna ya kutangaza biashara zao na umuhimu wa kusajili biashara zao ili ziweze kutambulika kisheria.

Maonesho haya ya Viwanda Vidogo (SIDO) ni ya kwanza Kitaifa yakiwa na Kauli Mbiu “Pamoja Tujenge Viwanda Kufikia Uchumi wa Kati” ambayo yalianza Oktoba 23, 2018 yatahitimishwa Oktoba 28, 2018.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/10/naibu-waziri-mabula-ashauri-wizara-ya.html

 

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa