• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Naibu Waziri Ikupa atoa wito kwa wenye Ulemavu kujiunga na CHF Iliyoboreshwa

Posted on: February 25th, 2019

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe.Stella Ikupa ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya watu wenye ulemavu, kuwahamasisha wanachama wao kujiunga na mfuko wa afya ya jamii (CHF )ulioboreshwa ili waweze kupata uhakika wa matibabu.

IKUPA ametoa wito huo wilayani Itilima katika ziara yake wakati akizungumza na viongozi wa Wilaya, Viongozi wa Vyama vya wenye ulemavu na  baadhi ya wenye ulemavu wenyewe wakati wa ziara yake wilayani humo Februari 25, 2019, ambayo ililenga kukagua utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ikiwa ni pamoja na mradi wa Kitalu nyumba na masuala mbalimbali yahusuyo wenye walemavu.

Amesema ni vema viongozi wa vyama na wenye ulemavu wakapena taarifa na kuhamasishani kujiunga na mfuko wa Afya ya Jamii(CHF) ulioboreshwa, ili wapewe vitambulisho waweze kutibiwa kirahisi.

“Mkijiunga na CHF iliyoboreshwa mkapata kadi mtakuwa na uwezo wa kutibiwa muda wowote, kwa hiyo peaneni hizo taarifa mjiunge watu mnaofahamiana muweze kupewa hivyo vitambulisho mpate kutibiwa kirahisi wakati tukiwa tunasubiri ile bima ya afya kwa kila Mtanzania” alisema Mhe. Ikupa.

Katika hatua nyingine amewaagiza maafisa Ustawi wa jamii na maendeleo ya jamii kutoa elimu vijijini kwa watu wenye ulemavu kuhusiana na uundwaji wa vikundi na namna ya kutekeleza miradi mbalimbali.

Mkuu wa Wilaya ya Itilima,Mhe.  Benson Kilangi akizungumzia utekelezaji wa mradi wa kitalu nyumba amesema katika awamu ya kwanza jumla ya vijana 20 wamepata mafunzo ya utengenezaji wa vitalu nyumba na kufundishwa stadi mbalimbali za kuendesha kilimo biashara na kuongeza mnyororo wa thamani.

Naye Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Festo Kiswaga amesema  miradi ya vitalu katika Mkoa wa Simiyu itatekelezwa kwa viwango na kwa malengo yaliyokusudiwa, huku akibainisha kuwa vitasaidia kuongeza kipato kwa wananchi katika mkoa  na kuwa sehemu ya wananchi kujifunza kilimo bora.

Kwa upande wao viongozi pamoja na watu wenye ulemavu walioshiriki katika ziara hiyo wamemwomba Mhe. Naibu Waziri kushughulikia baadhi ya changamoto zinazowakabili katika maeneo yao.

“Ninaomba Serikali itusaidie tuweze kupata wakalimani wa lugha ya alama ili na sisi walemavu wa kusikia tuweze kupata ujumbe unaokuwa unawasilishwa na viongozi wetu kwenye mikutano na ziara kama hii ya leo hii itatusaidia sana” alisema Mhandi Ntobi Mwenyekiti wa Chama cha Walemavu wasiosikia Mkoa wa Simiyu.

“NaombaWataalam waje watutembelee kwenye vijiji vyetu na kwenye vyama vyetu watusaidie kutupa elimu ya namna ya kuunda vikundi na namna ya kufanya shughuli zinazoweza kutuongezea kipato” Bw. Seni Jitabo mlemavu wa viungo Mkazi wa Zagayu wilayani Itilima.

Naibu Waziri Ikupa, anaendelea na ziara yake Mkoani Simiyu ambayo itahitimishwa 27 Februari 2019, akiwa wilayani Itilima Naibu waziri ametembelea kitalu nyumba kilichopo Lagangabilili na kituo cha maarifa ya jamii Kanadi, ambako amejionea shughuli mbalimbali za uzalishaji zinazofanywa na vijana.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/02/naibu-waziri-ikupa-atoa-wito-kwa-wenye.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa