• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Naibu Katibu Mkuu Mpanju Apoingeza Simiyu Kukubali kuwa Mwenyeji Siku ya Watu Wenye Ulemavu Kitaifa 2018

Posted on: June 25th, 2018

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. Amon Mpanju ameupongeza uongozi wa Mkoa wa Simiyu kwa namna unavyojishughulisha na masuala ya watu wenye ulemavu na kukubali kuwa mwenyeji wa Siku ya watu wenye Ulemavu Kitaifa inayotarajiwa kufanyika Desemba 03 mwaka huu mjini Bariadi.

Mpanjo ameyasema hapo alipomtembelea Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka ofisini kwake leo Juni 25 mara baada ya kufungua semina elekezi kuhusu Sheria ya Msaada wa Kisheria na kanuni zake kwa wasaidizi wa msaada wa kisheria mkoani humo.

"Ninawapongeza sana kwa kuwajali watu wenye ulemavu, mmekuwa wenyeji wa siku ya watu wenye ualbino mwaka huu, mmekubali kuwa wenyeji wa siku ya watu wenye ulemavu mwaka uliopita na mwaka huu tena mwezi Desemba, binafsi nawashukuru sana Simiyu" alisema.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema maadhimisho ya siku ya watu wenye ulemavu mwaka 2017 yaliyofanyika mkoani humo, lakini Simiyu imekubali kuwa mwenyeji tena kwa mwaka 2018 ili kujipanga upya na kuyafanya maadhimisho hayo kuwa ya tofauti.

"Mwaka jana tulifanya maadhimisho ya watu wenye ulemavu Kitaifa hapa Simiyu lakini nilitamani tukio hili lifanyike katika ukubwa wake, kwa dhamira hii hii mwaka 2018 tumekubali kuwa wenyeji ili tuyaandae maadhimisho haya tena kama tukio kubwa ambalo litahusisha watu wengi na kufanyika kwa uzito wake tofauti na mwaka jana" alisema Mtaka.

Mtaka amesema ameongea na viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kuona uwezekano kwa watu wenye ulemavu kufanya shughuli mbalimbali na kuonesha kazi mbalimbali wanazofanya, wiki moja kabla ya kilele ambacho kitakuwa Desemba 03, 2018.

Aidha, amesema pamoja na kuweka mipango ya watu wenye ulemavu kuonesha kazi zao kabla ya kilele pia upo mpango wa kuwashirikisha katika michezo mbalimbali ili waweze kuonesha vipaji vyao katika michezo.

Ameongeza kuwa dhamira ya Mkoa wa Simiyu pia ni kuwa kongamano kabla ya kilele ambalo litatoa fursa ya kufanya  mijadala kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo masuala kitaaluma, ujasiriamali, stadi za maisha na mengine ambayo yatawaleta pamoja watu wenye ulemavu kutoka maeneo tofauti.

Mgeni rasmi katika siku ya watu wenye ulemavu ambayo inatarajiwa kuadhimishwa Kitaifa Mjini Bariadi Mkoani Simiyu, anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa.

MWISHO

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa