• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa Awaongoza Viongozi na Wananchi Simiyu Mazishi ya Diwani Mahega

Posted on: June 14th, 2018

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Taifa, Dkt. Edmund B. Mndolwa amewaongoza viongozi wa CCM Taifa na Mkoa wa Simiyu, viongozi wa Serikali Mkoa wa Simiyu na wananchi wa Wilaya za Meatu na Maswa katika mazishi ya aliyekuwa Diwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu Kata ya Tindabuligi Marehemu Mahega Selemani Kijiji cha Zebeya wilayani Maswa, ambaye alifariki dunia Juni 10 katika ajali iliyotokea kwenye msafara wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James katika Kijiji cha Kisesa wilayani Meatu.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Dkt. Mndolwa ametoa pole kwa familia ya marehemu Mahega na akawaomba ndugu na familia kuwa na subira katika kipindi kigumu walichonacho.

Amesema Mhe. Rais anatoa shukrani kwa Kituo cha Afya Mwandoya, Hospitali Teule ya Mkoa wa Simiyu, Hospitali ya Rufaa Bugando na Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa namna walivyowahudumia majeruhi 19 wa ajali hiyo ambapo baadhi yao walitibiwa na kuruhusiwa na wengine bado wanaendelea kupata matibabu.

Aidha, Dkt. Mdolwa amemshukuru Mbunge wa Kisesa ambaye pia ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina kwa kuchukua maamuzi ya haraka ya kukodi ndege iliyowapeleka majeruhi tisa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, kwa ajili ya matibabu na uchunguzi zaidi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Mhe. Kheri James ametoa pole kwa familia, ndugu, wananchi wa Tindabuligi na kuwashukuru viongozi wa Mkoa wa Simiyu kwa msaada walioutoa toka siku ile ajali ilipotokea katika kuhakikisha wanasaidia kunusuru maisha ya wote waliojeruhiwa katika ajali ile.

"Ninawashukuru sana viongozi wa Mkoa wa Simiyu kwa namna walivyolishughulikia suala hili, kila niliyempigia simu baada ya ajali juhudi zake zilionekana; kwa kweli Simiyu mmedhihirisha ukamilifu wa mapenzi, ushirikiano na moyo wa kusaidia wengine"'alisema Kheri James.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akitoa pole kwa familia, ndugu na Baraza la Madiwani Meatu amewashukuru viongozi wa Chama na Serikali ambao wametoa misaada mbalimbali katika kuhakikisha majeruhi wa ajali wanapata matibabu kwa wakati na marehemu anasitiriwa kwa heshima zote kama kiongozi.

Katika hatua nyingine Mtaka amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kuhakikisha kuwa stahili zote za kisheria ambazo familia ya marehemu inapaswa kupewa na Halmashauri, zitolewe mapema badala ya kusubiri kufuatwa na familia hiyo.

Naye Waziri wa Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kisesa iliko kata aliyokuwa anaitumikia marehemu Mahega amewashukuru viongozi wa Chama na Serikali kwa namna walivyojitoa katika kushughulikia majeruhi na msiba ambapo pia amewashukuru wananchi wa Wilaya ya Meatu na Maswa mahali alikozikwa marehemu kwa ushirikiano na upendo mkubwa waliounesha katika msiba huo tangu siku Mhe. Mahega alipofariki mpaka kuzikwa kwake.

Mpina ametoa pole kwa familia, wananchi wa kata ya Tindabuligu na Wilaya ya Meatu kwa ujumla kwa kuondokewa na Mhe. Mahega ambaye amesema ameacha pengo kubwa kwa kuwa alikuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya wananchi na Meatu kwa ujumla.

Kwa upande wake Diwani wa Viti maalum Mhe. Avelina Kyakwambala ambaye amefanya kazi na Marehemu kama madiwani toka mwaka 2000 , amesema msiba huo umeupokea kwa masikitiko makubwa na kwamba Meatu imepoteza diwani mwadilifu, mchapakazi, anayezingatia kanuni zote za baraza, chama chake na alikuwa tayari kukosoa na kukosolewa kwa ajili ya kujenga na kuleta maendeleo kwa wananchi.

Msiba wa Marehemu Mahega Selemani ambaye  ameacha mke na watoto 14, umehudhuriwa na Wajumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Viongozi wa CCM Mkoa wa Simiyu, Simiyu na Mwanza na Viongozi wa Serikali Mkoa wa Simiyu na wilaya zote mkoani humo.

MWISHO



Jeneza lenye mwili wa Marehemu Mahega Selemani aliyekuwa Diwani wa Kata ya Tindabuligi Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu,  ambaye alifariki kwa ajali kwenye Msafara wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James Juni 10, 2018 katika Kijiji cha Kisesa wilayani Meatu , likiwekwa kaburini tayari kwa mazishi ambayo yamefanyika Kjiji cha Zebeya Wilayani Maswa.

Kutoka kulia Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Dkt. Joseph Chilongani, Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Benson Kilangi wakiweka shada la maua katika kaburi la Marehemu Mahega Selemani aliyekuwa Diwani wa Kata ya Tindabuligi katika Halmashauri hiyo mkoani Simiyu,  ambaye alifariki kwa ajali kwenye Msafara wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James Juni 10, 2018 katika Kijiji cha Kisesa wilayani Meatu , wakati wa mazishi yaliyofanyika Kjiji cha Zebeya Wilayani Maswa.

Kutoka kushoto Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe  Anthony Mtaka, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Bw. Erasto Sima na Mbunge wa Jimbo la Meatu, Salum Khamis wakiteta jambo  katika Msiba wa Marehemu Mahega Selemani aliyekuwa Diwani wa Kata ya Tindabuligi Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu,  ambaye alifariki kwa ajali kwenye Msafara wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James Juni 10, 2018.

Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James akiweka shada la maua katika kaburi la Marehemu Mahega Selemani aliyekuwa Diwani wa Kata ya Tindabuligi Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu,  ambaye alifariki kwa ajali kwenye Msafara wake akiwa ziarani Mkoani humo, Juni 10, 2018 katika Kijiji cha Kisesa wilayani Meatu , wakati wa mazishi yaliyofanyika Kjiji cha Zebeya Wilayani Maswa.

Kutoka kushoto Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe  Anthony Mtaka, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Bw. Erasto Sima wakiteta jambo  katika Msiba wa Marehemu Mahega Selemani aliyekuwa Diwani wa Kata ya Tindabuligi Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu,  ambaye alifariki kwa ajali kwenye Msafara wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James Juni 10, 2018 katika Kijiji cha Kisesa wilayani Meatu , wakati wa mazishi yaliyofanyika Kjiji cha Zebeya Wilayani Maswa.

Mjane wa marehemu Mahega Selemani aliyekuwa Diwani wa Kata ya Tindabuligi Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu,  ambaye alifariki kwa ajali kwenye Msafara wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James Juni 10, 2018  katika Kijiji cha Kisesa wilayani Meatu, akiweka shada la maua kwenye kaburi la mume wake wakati wa mazishi yaliyofanyika Kjiji cha Zebeya Wilayani Maswa.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe  Anthony Mtaka akiweka shada la maua katika kaburi la Marehemu Mahega Selemani aliyekuwa Diwani wa Kata ya Tindabuligi Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu,  ambaye alifariki kwa ajali kwenye Msafara wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James Juni 10, 2018 katika Kijiji cha Kisesa wilayani Meatu , wakati wa mazishi yaliyofanyika Kjiji cha Zebeya Wilayani Maswa.

Baadhi ya waombolezaji katika Msiba wa Marehemu Mahega Selemani aliyekuwa Diwani wa Kata ya Tindabuligi Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu,  ambaye alifariki kwa ajali kwenye Msafara wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James Juni 10, 2018, katika Kijiji cha Kisesa wilayani Meatu kabla ya mazishi yaliyofanyika Kjiji cha Zebeya Wilayani Maswa

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Khadija Shaban maarufu kama Keisha akizungumza na waombolezaji katika Msiba wa Marehemu Mahega Selemani aliyekuwa Diwani wa Kata ya Tindabuligi Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu,  ambaye alifariki kwa ajali kwenye Msafara wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James Juni 10, 2018 katika Kijiji cha Kisesa wilayani Meatu, kabla ya mazishi yaliyofanyika Kjiji cha Zebeya Wilayani Maswa.

Mbunge wa Viti maalum( CCM) Mkoa wa Simiyu akiweka shada la maua katika kaburi la Marehemu Mahega Selemani aliyekuwa Diwani wa Kata ya Tindabuligi Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu,  ambaye alifariki kwa ajali kwenye Msafara wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James Juni 10, 2018 katika Kijiji cha Kisesa wilayani Meatu , wakati wa mazishi yaliyofanyika Kjiji cha Zebeya Wilayani Maswa.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa