• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Mwenyekiti wa CCM Mkoa Aishauri Serikali Kuzipa Kipaumbele Wilaya Mpya Simiyu Ujenzi wa Ofisi na Makazi

Posted on: April 11th, 2018

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo ameishauri Serikali kutoa kipaumbele kwa wilaya mpya za Busega na Itilima mkoani humo,  katika Ujenzi wa Ofisi na Nyumba za Watumishi ili watumishi waweze kufanya kazi katika mazingira mazuri.

Mhe. Yakobo ameyasema hayo leo alipotembelea na kuona Ujenzi wa Jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Busega ambalo mpaka kukamilika kwake litagharimu shilingi bilioni 4.6 , wakati wa Ziara ya Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa ya kukagua Utekelezaji wa Ilani ya CCM wilayani humo.

“Ingekuwa vizuri Ofisi na nyumba za watumishi zipatikane maana Busega imeshajitegemea, kama mkoa tuwe na kaulimbiu hiyo kuwa wilaya hizi mpya ziangaliwe; eneo hili ni changa linapaswa kuendelezwa ili watumishi wa hapa nao wafurahie utumishi wao”alisema Mhe.Yakobo

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema Serikali ya Mkoa kwa kushirikiana na Wakurugenzi wa Halmashauri waliwasilisha suala hilo kwa Kamati ya Bunge na kuomba mkoa wa Simiyu kwa kuwa ni mpya uangaliwe sana kwenye mahitaji muhimu hususani yanayowagusa watumishi ikiwemo makazi.

“Ningependa kuwaomba Mwenyekiti wa CCM mkoa na Mjumbe wa NEC mlibebe jambo hili kama agenda ya Mkoa, sisi kama Serikali tulienda pamoja na Wakurugenzi kwenye Kamati ya Bunge, tukaomba kama Mkoa mpya waangalie mahitaji ya msingi hasa kwa watumishi, majengo yote haya tumeyaombea fedha na majengo ya Mkoa pia tumeyaombea fedha” alisema Mtaka.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg. Jumanne Sagini amesema Serikali imeshajenga nyumba nne (04) kwa ajili ya watumishi wa Halmasahuri ya Wilaya ya Busega na mpango wa kuendelea kupata fedha kwa ajili ya kujenga nyumba zilizobaki unaendelea.

Aidha, Sagini amesema Serikali imetenga fedha  kwa ajili ya kukamilisha jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega pamoja makazi yake

Katika hatua nyingine Sagini amewataarifu wajumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Simiyu kuwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo na  kukamilisha ujenzi wa Nyumba za Viongozi wa Mkoa zimetengwa.

Kamati ya Siasa ya CCM  Mkoa ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa Mhe.Enock Yakobo pamoja na kukagua jengo la Halmashauri wilayani Busega ilikagua Miradi mingine ya maendeleo katika Sekta ya Maji, Elimu na Afya.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA HAPA:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/04/mwenyekiti-wa-ccm-simiyu-aishauri.html

 


Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa