• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Mtaka:Simiyu Itakuwa Balozi Mzuri wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya

Posted on: February 18th, 2017

Na Stella Kalinga

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amesema kuwa ushirikiano uliopo kati ya Ofisi yake,Wakuu wa Wilaya ,Wakurugenzi wa Halmashauri, utaufanya mkoa huo kuwa balozi mzuri kwa wananchi kujiunga kwenye mfuko Taifa wa Bima ya Afya.

Mtaka ameyasema hayo wakati wa Mkutano wa wadau wa Mfuko wa Bima ya afya (NHIF) uliofanyika katika ukumbi wa Kanisa Katolini na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa Bodi ya mfuko huyo Taifa Anne Makinda, ambao ulikuwa na lengo kubaini changamoto zinazowakabili wanachama wa Mfuko huo sambamba na utoaji wa elimu juu ya umuhimu wa kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya afya. Amesema kuwa wananchi kujiunga na mfuko huo ni muhimu sana kwani watapunguza gharama kubwa wakati wa matibabu na wanapaswa kutambua kuwa ugonjwa huingia mwilini bila taarifa.

“..Ushirikiano tutakaoonesha sisi viongozi juu ya uhamasishaji wa wananchi kujiunga na mfuko wa bima ya afya utawasaidia wananchi kuokoa gharama kubwa ya fedha wakati wa kupata matibabu…na kujiunga uanachama ndio njia pekee rahisi na kisasa katika kupata matibabu duniani kote…Alisema

Aidha Katika kufikia dhamira ya serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Pombe Magufuli ya Tanzania ya viwanda na kuwa na nguvu kazi iliyo salama kiafya, ameiomba Bodi ya Mfuko huo wa Bima ya afya kuanzisha ofisi za Mkoa, ili kuwarahisishia wananchi wa mkoa huo upatikanaji wa huduma.

Awali akitoa taarifa ya Maboresho ya huduma kwa wanachama na wadau wa mfuko wa Bima ya afya Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Bima ya afya Taifa Leonard Konga alieleza kuwa Mfuko huo umeanzishwa kwa dhamira ya kutoa Bima ya afya kwa makundi mbalimbali ya wananchi, Kujenga uwezo wa kifedha kwa vituo na kushirikisha sekta binafsi katika kuharakisha maendeleo ya sekta ya afya.

Konga alitaja mafanikio ya utekelezaji wa shughuli za Bima ya afya yanategemea kila mdau kutimiza wajibu wake kwani mazingira ya kiutendaji ni kusimamia na kutekeleza miongozo na maagizo ya serikali kupitia wizara yenye dhamana ya kusimamia upatikanaji wa huduma za afya. Alibainisha kuwa lengo mahususi katika utekelezaji wa mpango wa Mfuko wa Bima ya afya kuw ni pamoja na kuwawezesha wananchi wengi zaidi kupata huduma za afya kuanzia ngazi ya Zahanati hadi ngazi ya hospitali ya Mkoa na Kuongeza wigo mpana zaidi kwa watanzania wanaopata huduma za matibabu kupitia Bima ya Afya. Naye Kaimu Meneja wa wa Bima ya afya Mkoa wa Simiyu ambaye pia ni Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya afya Mkoa wa Shinyanga Immanuel Imani alizitaja changamoto zinazowakabili ikiwa ni pamoja na Upungufu wa dawa katika baadhi ya vituo, Ukosefu wa vifaa tiba na ubovu wa majengo, waajiri kuchelewesha madai pamoja na uchache wa watoa huduma.

Hata hivyo Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Bima ya afya Taifa (NHIF) amesema kuwa katika maeneo mengi aliyopita amebaini kuwa wananchi wengi wanatumia fedha zao kujiunga na Mfuko wa Bima ya Afya lakini wanapoenda kuhudumiwa wanakumbana na matusi pasipo kupata huduma bora.

Amesema kuwa Bodi yake imekusudia kuboresha huduma za matibabu kwa wananchi sambamba na kupinga vikali lugha chafu zitolewazo na baadhi ya watoa huduma katika sekta ya afya dhidi ya wananchi wanaoenda kupata matibabu katika Zahanati, Vituo vya afya, Hospitali za Wilaya, Mikoa na Rufaa.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa