• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Mtafiti TPRI Aainisha Sababu za Viuatilifu Kushindwa Kuua Wadudu Kwenye Pamba

Posted on: November 12th, 2020

Matumizi ya viuatilifu chini ya kiwango kilichoelekezwa, matumizi yasiyo sahihi ya viuatilifu,unyunyiziaji na utunzaji wa viuatilifu usio sahihi na uwezo mdogo wa wakulima kutambua visumbufu vya mazao,vimetajwa kuwa ni miongoni mwa sababu za viuatilifu kushindwa kuua wadudu katika zao la pamba.

Hayo yamebainishwa na Mtafiti wa kudhibiti visumbufu vya mazao/mimea kutoka Taasisi ya Utafiti wa viuatilifu nchini(TPRI), Bw. Ramadhan Kilewa wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya taaluma maalum kwa watoa huduma ya unyunyiziaji wa viuatilifu kwa zao la pamba mkoani Simiyu jana Novemba 11, 2020 mjini Bariadi.

“TPRI imeamua kabla ya msimu kuanza tuwajee uwezo wadau wetu ili wakafanye kazi nzuri itakayoleta tija katika uzalishaji wa pamba; tumeanza na wadau wanaofanya kazi mashambani ili tuwawezeshe kuwa na mbinu sahihi za kuchagua viuatilifu vilivyyo sahihi, utunzaji sahihi wa viuatilifu na utupaji wa viwekeo tupu kwa kufuata taratibu ili wasilete madhara kwa binadamu, wanyama na mazingira,” alisema Bw. Kilewa.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yanalenga kutimiza takwa la kisheria la Sheria Namba 4 ya Afya ya Mimea ya mwaka 2020 sehemu ya 37 inayosisitiza mafunzo ya usimamizi na udhibiti wa viuatilifu ili kuhakikisha mazao yatokanayo na kilimo na mifugo yanayoweza kutumika na wadau nchini yawe safi na yasiwe na mabaki yenye madhara kwa afya binadamu.

Akifungua mafunzo hayo Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi, Miriam Mmbaga ametoa wito kwa watoa huduma ya unyunyiziaji wa viuatilifu kwa zao la pamba kutekeleza jukumu hilo kwa kuwasaidia wakulima kwa mujibu wa sheria na maelekezo waliyopewa huku akiwaasa kutowapotosha na kuwaibia wakulima.

Aidha, Mmbaga amezitaka Halmashauri zote mkoani Simiyu kuhakikisha zinaandaa maafisa Kilimo watakaowasimamia watao huduma hao na kusisitiza watoa huduma hao kutambulishwa kwa maafisa kilimo wa kata  na kwa wakulima wa pamba katika vijiji ili waeze kutambulika na kufikiwa kwa urahisi wanapohitajika kutoa huduma ya unyunyiziaji.

Kaimu Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bibi, Kija Kayenze amesema, mara baada ya mafunzo haya matarajio mkoa ni kuongeza tija ya uzalishaji wa pamba mwaka huu kutoka wastani wa kilo 175 mpaka kilo 450 kwa ekari; ambapo amebainisha kuwa tija ndogo ilichangiwa na kukosa elimu ya matumizi sahihi ya viuatilifu.

Jumla ya vijana 600 mkoani Simiyu wanatarajiwa kunufaika na mafunzo ya taaluma maalum ya huduma ya unyunyiziaji wa viuatilifu kwa zao la pamba.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/11/mtafiti-tpri-aainisha-sababu-za.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa