• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Mkurugenzi TRL Awataka Vijana Kuwa na Ndoto Zitakazowasaidia Kufika Fursa za Kujikwamua Kiuchumi

Posted on: September 16th, 2018

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania, Bw. Masanja Kadogosa amewataka vijana hapa nchini kuwa ndoto ili waweze kuona na kuzifikia fursa mbalimbali zilizopo na kukuza Uchumi wao na Taifa kwa ujumla, kupitia uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika Sekta mbalimbali.

Kadogosa ameyasema hayo Septemba 14, 2018 wakati akizungumza na Vijana wa Mkoa wa Simiyu, katika Kongamano la Vijana wa Mkoa wa huo lililoandaliwa na Asasi ya  Wanafunzi wa Vyuo Vikuu na Waliohitimu wanaotoka mkoa wa Simiyu- Simiyu University Students  and Associates Association (SUSAA), lililofanyika Mjini Bariadi .

Amesema Serikali imewekeza fedha nyingi  katika sekta ya viwanda, nishati, ujenzi wa miundombinu kama reli ya kisasa, barabara na miundombinu ya usafiri wa anga na majini kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu,  hivyo vinana wanapaswa kuwa na ndoto zitakazowawezesha kuziona fursa ili wajikwamue kiuchumi.

“Ni jambo muhimu sana kwa vijana kuwa na ndoto kwa sababu wakiwa na ndoto wataona fursa, ndoto zitawasaidia kufikiria namna ya kujiwekea malengo; Serikali imewekeza kwenye vitu vingi sana na kutengeneza mazingira wezeshi, ni wakati wao sasa vijana kutambua nafasi yao katika kuzitumia fursa hizo” alisema

Aidha, Kadogosa ameshauri makongamano ya Vijana kama lililofanyika Mkoani Simiyu yafanyike pia katika mikoa mingine na akatoa wito kwa Viongozi na watu mbalimbali wawe tayari kutoa elimu, ushauri, uzoefu ili kuwajengea uwezo vijana hapa nchini.

Awali akifungua Kongamano hilo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amewataka vijana wa mkoa huo kufuata nyayo za wazazi wao katika kuweka jitihada kwenye kilimo ambapo uzalishaji wa pamba mwaka 2018 umefikia takribani kilo milioni 140 kutoka kilo 70 za msimu uliopita.

Aidha,  Kiswaga amesema vijana hao wajiandae pia katika uwekezaji kwenye viwanda “Sasa hivi Serikali inaenda kwenye viwanda na hapa naviona viwanda vingi sana hapa naviona viwanda viwanda vya nguo, naviona viwanda vidogo vingi sana kutoka kwenu, kwa hiyo tujiandae  katika kuhakikisha mkoa huu tunawekeza na wawekezaji ni sisi tuliopo kwenye kongamano hili”.

Kwa upande wake Waziri wa Uvuvi na Mifugo, Mhe.  Luhaga Mpina, ambaye alikuwa miongoni mwa watoa mada katika kongamano hilo, amewataka vijana hususani wahitimu wa Vyuo Vikuu  kutumia fursa zilizopo hapa nchini hususani katika sekta ya Kilimo, Uvuvi na Ufugaji  kujiajiri badala ya kusubiri kuajiriwa.

Awali akisoma risala kwa niaba ya Vijana wa Mkoa wa Simiyu na  Viongozi wa SUSAA, Mwenyekiti wa SUSAA Kanda ya Mashariki, Bw. Musa Joseph amesema lengo kuu la kongamano hilo ni kuwakutanisha vijana pamoja ili kueleweshana juu ya dhana ya uchumi wa viwanda nchini na namna kila kijana anavyoweza kushiriki kwa vitendo katika eneo lake.

Nao baadhi ya Vijana wakiongelea Kongamano hilo wamesema kuwa limewasaidia fursa kubwa kwao ya wao kupata elimu, ujuzi, na kugundua fursa za uwekezaji na  kujiajiri wenyewe badala ya kusubiri kuajiriwa.

“ Kongamano hili limetusaidia sana sisi vijana kugundua fursa nyingi za kuwekeza, kujiajiri ambazo vijana wengi bado hawajaweza kuzitumia katika kuhakikisha wanajiletea maendeleo, naamini kupitia elimu tuliyoipata leo tutazitumia vizuri fursa zilizopo, ili tujiletee maendeleo” alisema Emmanuel Lyaganda

Kongamano hili lilihusisha vijana kutoka maeneo tofauti wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali  na limeandaliwa na Asasi ya Vijana walioko Vyuo Vikuu na waliohitimu ambao ni wakazi wa mkoa wa Simiyu- Simiyu University Students  and Associates Association(SUSAA), likiwa na Kauli mbiu isemayo “ VIJANA NA UWEKEZAJI KATIKA KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA TANZANIA”.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/09/mkurugenzi-trl-awataka-vijana-kuw-na.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa