• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Mkoa wa Simiyu waweka Mikakati Kuboresha Hali ya Lishe

Posted on: June 29th, 2018

Mkoa wa Simiyu umejiwekea mikakati mbalimbali kuboresha hali ya lishe mkoani humo ikiwa ni pamoja na kukabiliana na tatizo la utapiamlo kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano.

Hayo yamesemwa na Mratibu wa Lishe Mkoa wa Simiyu, Dkt. Chacha Magige katika kikao cha kamati ya lishe kilichofanyika katika Ukumbi wa Hospitali Teule ya Mkoa, Mjini Bariadi.

Chacha amesema elimu inatolewa kwa wananchi hususani akina mama wajawazito na wanaonyonyesha juu ya umuhimu  kula vyakula vinavyotokana na makundi yote matano na kuhakikisha kuwa elimu ya lishe kwa akina mama inatolewa katika kliniki ya mama na mtoto na vidonge vya madini Chuma na Folic Acid vinatolewa

Aidha, amesema elimu ya uandaaji na uhifadhi wa vyakula vinavyotoa virutubishi vya kutosha; mfano, ufundikaji na uchachushaji wa vyakula inatolewa na mpango mkakati wa lishe wa Mkoa utakaowezesha kutambua changamoto mbalimbali za lishe, na kuzipatia ufumbuzi, na hatimaye kubadilisha hali ya lishe ilivyo unakamilishwa kwa wakati.

Ameongeza kuwa Idara ya Afya itatumia maonesho ya NaneNane yatakayofanyika Kitaifa Mkoani Simiyu kuelimisha jamii juu ya wakina mama kuwanyonyesha watoto maziwa ya mama mara tu baada ya kuzaliwa, kunyonyesha watoto maziwa ya mama pekee kwa muda wa miezi sita ya mwanzo na baada ya hapo kuwaanzishia vyakula vya nyongeza.

Pamoja na elimu ya masuala ya lishe, Chacha amesema elimu juu ya uzazi wa mpango inahitajika kwa wanachi ili kuwasaidia kupata uelewa wa umuhimu wa kuwa na idadi ya watoto watakaoweza kuwahudumia kwa mahitaji ya muhimu ikiwepo chakula bora.

Mwakilishi wa Shirika la CUAMM Bw. Zacharia Msumari amesema shirika hilo limekuwa likitoa tiba ya vyakula (tiba lishe)  kwa watoto wenye utapiamlo katika baadhi ya vituo vya kutolea huduma za afya mkoani humo na kuwawezesha baadhi yao kuwa katika hali nzuri.

Ameongeza kuwa shirika hilo pia imekuwa likitoa elimu kwa watoa huduma katika vituo vya kutolea huduma za afya ili nao waweze kuelimisha wazazi na walezi namna ya kukabiliana na utapiamlo kwa kuwalisha watoto vyakula vya makundi yote matano ambavyo vinapatikana katika maeneo yao ili kuimarisha afya zao.

Awali akifungua kikao hicho Kaimu Katibu  Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Mashaka Luhamba ametoa wito kwa wadau wa afya kuendelea kutoa elimu katika jamii juu ya uandaaji wa vyakula katika familia ambavyo vinajumuisha makundi yote matano ya vyakula , kutokana na mkoa wa Simiyu kuzalisha aina mbalimbali za vyakula.

MWISHO

Baadhi ya wadau wa afya na wajumbe wa  Kamati ya Lishe ya Mkoa wa Simiyu, wakimsikiliza Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Mashaka Luhamba  katika Kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Mjini Bariadi.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa