• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Mhifadhi Mkuu Serengeti:Ujenzi wa Uwanja wa Ndege Simiyu Utaongeza Huduma za Utalii

Posted on: May 17th, 2018

Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA), William Mwakilema amesema Uwanja wa Ndege Simiyu unaotarajia kujengwa  Eneo la Igegu wilayani Bariadi utakapokamilika  utaongeza huduma za Utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Mwakilema ameyasema hayo wakati  ziara ya Balozi wa Indonesia  hapa nchini , Prof.Dkt. Ratlan Pardede na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mei 16  ili kujionea wanyama na vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo.

Amesema Hifadhi ya Serengeti ina uwanja ambao unaowezesha ndege ndogo kutua hivyo, ujenzi wa uwanja wa Simiyu utakaowezesha  ndege kubwa kutua itakuwa ni nyongeza ya huduma, ambapo  ndege kubwa zitakapotua Simiyu watalii ambao hawawezi kutembea mwendo mrefu kwa kutumia magari, watachukuliwa na ndege ndogo kutoka Simiyu na  kupelekwa  Seronera(Serengeti).

Ameongeza kuwa,  kuwepo kwa uwanja huo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma za Utalii, ambapo wafanyabiashara wengi  wa huduma za Utalii watavutiwa kuwekeza mkoani Simiyu kwa ajili kutoa huduma kwa wageni watakaotua uwanjani hapo na wanaoenda kufanya utalii Serengeti.

Aidha, Mwakilema amesema Mamlaka ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti inaendelea kushirikiana na Mkoa wa Simiyu kuhakikisha kuwa rasilimali zote ndani ya hifadhi ziko salama na zinaendelea kutunzwa ili  Taifa liweze kunufaika kiuchumi kupitia utalii.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Mpango wa Mkoa huo ni kufikisha kwa wepesi huduma za Utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti hivyo mkoa umepanga kujenga uwanja huo wa ndege katika Eneo la Igegu wilayani Bariadi ambalo liko karibu kabisa na Hifadhi hiyo.

“Tumepanga kujenga Uwanja wa Ndege pale Igegu ili kufikisha huduma za utalii kwa wepesi katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na mwaka huu wa fedha 208/2019  tumetengewa fedha kwa ajili ya ujenzi wa uwanja huo  utakaokuwa na ukubwa wa kilometa 2.5,  pia sisi kama mkoa tutahakikisha tunafungua malango yote ya watalii kuja kwenye vivutio vyetu” alisema Mtaka

“Tunapokamilisha miundombinu ya barabara ya Lamadi-Bariadi-Maswa-Mwigumbi ni pamoja na kuona namna tutakavyounganisha  ufunguaji wa barabara zitakazowezesha watu kwenda kwenye hoteli zote za kitalii zilizojengwa ndani ya hifadhi hasa zilizo katika eneo letu, ili huduma za utalii zirahisishwe” alisisitiza.

Kwa upande wake Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Prof. Dkt. Ratlan Pardede  baada ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti amesema atazungumza na Wafanyabiashara wa Indonesia na kuwaalika kuwekeza katika Sekta ya Utalii nchini Tanzania hususani Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, huku akisisitiza kutoa wito kwa wananchi wa Indonesia kutembelea Hifadhi ya Serengeti ili kuja kujionea vivutio mbalimbali vya utalii.

Balozi wa Indonesia, Prof. Dkt. Ratlan Pardede amehitimisha ziara yake kikazi mkoani Simiyu ambapo ameahidi kuimarisha ushirikiano kati ya Indonesia na Tanzania na hasa Mkoa wa Simiyu katika masuala ya kilimo na biashara ya zao la pamba, uwekezaji wa viwanda vya nguo, bidhaa za ngozi na mbolea pamoja na utalii.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/05/mhifadhi-mkuu-serengeti-uwanja-wa-ndege.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa