• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Mavunde Aagiza Halmashauri Kutenga Maeneo ya Uzalishaji Mali kwa Vijana, Wanawake

Posted on: August 2nd, 2020

Naibu Waziri ofisi ya waziri mkuu kazi, vijana na ajira Mhe. Anthony Mavunde ameziagiza halmashauri zote nchini kutenga maeneo maalum kwa ajili ya shughuli za uzalishaji mali kwa vijana na wanawake..

Naibu Waziri Mavunde ameyasema hayo Agosti 02, 2020 ambayo imetengwa maalum kwa ajili ya kuhamasisha Programu ya kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP)baada ya kutembelea mabanda ya maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020,  katika viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.

“Mhe. Waziri Mkuu wa awamu ya tatu alitoa maelekezo ya kutenga maeneo hayo, awamu ya nne akaja Mzee Pinda Novemba 2014 likaja azimio la kila mkoa kutenga maeneo maalum kwa ajili ya shughuli za uzalishaji mali kwa vijana na wanawake, mpaka sasa zimetengwa hekari 203,000 tu ambazo bado hazitoshi kulingana na ukubwa wa nchi yetu, kwa hiyo kuna baadhi ya mikoa ambayo haijatekeleza   ” alisema Mavunde

Mhe. Mavunde amesema Ofisi ya Waziri Mkuu inashirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI vijana wanawezeshwa kushiriki katika Kilimo kupitia mradi wa Vitalu nyumba ambapo vijana 100 kwa kila halmashauri wamepewa mafunzo na mpaka sasa vijana takribani 18,000 wamefikiwa lengo likiwa ni kuwafikia vijana huku lengo likiwa ni kuwafikia vijana 45,000 kwa awamu ya kwanza.

Ameongeza kuwa kwa sasa vijana wamehamasika sana kufanya shughuli za kilimo tofauti na ilivyokuwa siku za nyuma ambapo kilimo kinafanywa na watu waliokosa kazi nyingine, hivyo akaendelea kusisitiza maeneo maaluma kwa ajili ya shughuli mbalimbali za uzalishaji ikiwemo kilimo na kuwatafutia masoko ya bidhaa zao.

Katika hatua nyingine Mavunde ametoa kwa wananchi wote kujitokeza kwa wingi katika viwanja vya Nyakabindi Bariadi kujifunza teknolojia mbalimbali zitakazoongeza tija na thamani katika kazi wanazofanya ikiwemo kilimo, mifugo na uvuvi.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga amesema mkoa huo uko tayari kitoa maeneo kwa ajili ya shughuli za uzalishaji ikiwemo kilimo huku akiahidi kuendelea kushirikiana na Wizara ya Kilimo kuhakikisha Programu ya kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP) haibaki katika maandishi bali inaingia katika vitendo.

Naye  Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe amesema utekelezaji wa Programu ya kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP) unahitaji fedha hivyo akatoa rai kwa taasisi za fedha kuongeza fedha katika sektaya kilimo, mfugo na uvuvi ambazo zinagusa sehemu kubwa ya maisha ya watu, ambapo amesisitiza wizara ya kilimo, ofisi ya Waziri Mkuu na wizara ya fedha kulifanyia kazi hilo.

Maonesho ya nanenane Kitaifa mwaka 2020 ni ya tatu sasa katika Mkoa wa Simiyu ambapo Kauli Mbiu ya maonesho hayo mwaka huu ni “KWA MAENDELEO YA KILIMO , MIFUGO NA UVUVI CHAGUA VIONGOZI BORA 2020.”

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-http://simiyuregion.blogspot.com/2020/08/mavunde-aagiza-halmashauri-kutenga.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa