• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Malalamiko ya Wachimbaji, Wenye Mashamba Mgodi wa Bulumbaka Bariadi Yashughulikiwe: RAS Simiyu

Posted on: April 8th, 2021

Uongozi wa mkoa wa Simiyu umetoa siku saba kwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi na Ofisi ya Madini Mkoa wa Simiyu kupitia malalamiko na hoja zote za wachimbaji wadogo, wamiliki wa mashamba na wadau wengine katika mgodi wa dhahabu wa Bulambaka wilayani Bariadi na kuhakikisha shughuli za uchimbaji wa madini unafanyika kwa mujibu wa sheria.

Hayo yameelezwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga mara baada ya kiongozi huyo na viongozi wengine wa mkoa kuzungumza na wananchi hao waliofika  katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Aprili 08, 2021 Mjini Bariadi ili kupata ufumbuzi wa malalamiko yao.

“ Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Simiyu imepokea wachimbaji na wadau mbalimbali wanaofanya kazi katika mgodi wa Bulumbaka na kuwasikiliza baada ya kutoka kwa Mkuu wa Wilaya; hoja za wachimbaji ni pamoja na wao kutokubaliana na utaratibu wa utoaji leseni kwa kikundi kilichopewa leseni kufanya kazi katika eneo lile, ambapo baadhi ya wanakikundi wamedai kuwa hawakitambua kwa kuwa hawakushirikishwa,”

“Baada ya kuwasiliza pamoja na hoja nyingine tumeona hili suala bado liko ndani ya uwezo wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya hivyo nimetoa siku saba kwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya  na ofisi ya madini mkoa wa Simiyu, wapitie hoja zote na kutoa ushauri na kufanyia kazi yale yote wanayoweza kuyafanyia kazi kwenye ngazi yao kuhakikisha uchimbaji madini ufanyike kwa mujibu wa sheria,” alisema Mmbaga.

Nao baadhi ya wamiliki wa mashamba na wachimbaji wadogo ambao ni wananchi walioko eneo la mgodi la Bulumbaka wamesema:

“Baadhi ya wenye mashamba hawajui leseni hii ilivyopatikana maana hawakushirikishwa, sisi wananchi ambao pia ni wachimbaji wadogo tunaomba haki itendeke, hatutaki mtu yeyote anyanyaswe,” alisema Bw.Masuke Sahani mkazi wa Bulumbaka

“ Sisi tuna kilio kikubwa na mgodi wetu tumeshangaa kwamba Mwananyanzala amepata leseni wakati sisi tuna muda mrefu tunatafuta hiyo leseni kwa watu wa madini hatujapata, tunaomba Mkuu wa Wilaya atusaidie sisi wakazi wa Bulumbaka tupate haki yetu,” alisema Monica Daniel mmoja wa wamiliki wa mashamba Bulumbaka.

Awali akizungumzia na wananchi hao walipofika ofisini kwake, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amesema malalamiko ya wananchi hao ameyapokea, ambapo amebainisha kuwa maagizo aliyayatoa awali hayakufuatwa hivyo akawaomba wauone uongozi wa mkoa ambao nao baadaye ukaelekeza  ofisi yake iyashaghulikie kwa kuwa yako ndani ya uwezo wake.

Mmiliki wa leseni katika eneo la Bulumbaka Seni Mwananyanzala amesema kuwa leseni yake ilitolewa kihalali ambapo alifafanua kuwa leseni hiyo ilisainiwa tarehe 19 Machi 2021.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2021/04/malalamiko-ya-wachimbaji-wenye-mashamba.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa