• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Makamu wa Rais: Sheria Ndogo Zitungwe Kulinda Mabwawa ya Maji

Posted on: February 20th, 2018

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amemtaka Mkuu wa Wilaya ya Meatu Dkt.Joseph Chilongani pamoja na wataalam wa Halmashauri ya Meatu kutunga sheria ndogo zitakazosaidia kulinda na kutunza bwawa la maji la  Mwanjoro.

Mhe. Makamu wa Rais amesema hayo leo wakati akizungumza na wananchi wa kata ya Mwanjoro mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika Mradi wa bwawa la maji la Mwanjoro lililopo  kata ya Mwanjoro  Wilayani humo.

Mhe.Makamu wa Rais amesema  Serikali inatambua uwepo wa tatizo la maji na ukame uliopo Wilayani humo ndiyo maana imeamua kujenga bwawa hilo litakalogharimu shilingi bilioni1.3 kwa awamu ya kwanza,  hivyo ni lazima kuwepo na sheria ndogo zitasaidia kufanya bwawa hilo lidumu na kutoa huduma endelevu kwa wananchi

“Hili bwawa halitaki mifugo isogezwe huku wala shughuli za binadamu zije huku, nimemtaka Mkuu wa Wilaya na wataalam waweke sheria ndogo za kulinda bwawa na eneo linalozunguka bwawa, sheria zitakapo tungwa mzifuate, mkiliharibu mtakosa maji na mtarudi kule kule mlikotoka” alisisitiza Makamu wa Rais.

Ameongeza kuwa pamoja na Serikali kujenga Bwawa hilo kwa ajili ya matumizi ya binadamu na mifugo, kutokana na hali ya ukame ya wilaya hiyo Serikali imejipanga kujenga bwawa lingine litakalotumika kwa ajili ya shughuli za Kilimo cha Umwagiliaji.

Akitoa maelezo juu ya mradi huo, Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe amesema Sera ya Serikali ni kuwapunguzia wananchi adha ya kufuata maji umbali mrefu, hivyo kupitia mradi wa Mwanjoro wananchi wa Vijiji vya Mwanjoro, Mbushi na Jinamo watasogezewa huduma za maji karibu ili wasiende zaidi ya mita 400.

 Aidha,  amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Fabian Manoza  kuwasilisha orodha ya mahitaji ya visima vya maji katika wilaya hiyo,  ili viwekwe katika bajeti ya mwaka 2018/2019 , lengo likiwa ni kuongeza kiwango cha utoaji wa huduma za maji kwa wananchi wilayani humo.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Mbunge wa jimbo la Meatu Salum Khamis ameishukuru serikali kwa jitihada zote zinazofanyika katika kuondoa tatizo la maji na akaahidi kushirikiana na Wabunge pamoja na Wizara ya Maji kuhakikisha wananchi wa Meatu wanapata maji safi na salama.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kisesa ambaye pia ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe.Luhaga Mpina akizungumza kwa niaba ya wananchi katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Kata ya Mwandoya ameomba Wizara ya Maji isaidie upatikanaji wa maji katika kata zote za Jimbo la Kisesa.

Makamu wa Rais anaendelea na ziara yake ya siku nne Mkoani Simiyu ambapo leo akiwa wilayani Meatu ameweka Jiwe la msingi mradi wa Maji wa Bwawa la Mwanjoro, amesalimia wananchi wa Kata ya mwanjoro, Mwanhuzi na kufanya mkutano wa hadhara katika Kata ya Mwandoya.

MWISHO

KUPATA  PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA HAPA:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/02/makamu-wa-raissheria-ndogo-zitungwe.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa