• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Makamu wa Rais awapongeza Viongozi Simiyu kwa Kutekeleza Sera ya Tanzania ya Viwanda kwa Vitendo

Posted on: February 19th, 2018

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan amewapongeza viongozi wa Mkoa wa Simiyu kwa kuunga mkono jitihada za Serikali  hususani katika utekelezaji wa Sera ya Tanzania ya Viwanda. 

Mhe.Makamu wa Rais ametoa pongezi hizo wakati akizungumza na Wananchi wa Mji wa Bariadi kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa CCM Mkoa wa Simiyu.

Amesema amepokea taarifa kuwa Mkoa wa Simiyu una jumla ya viwanda 14 vya kuchakata pamba na viwanda vidogo vya kuongeza thamani ya mazao 1035,  jambo ambalo ni maendeleo makubwa kwa wananchi na akatoa wito kwa wananchi wa Simiyu kuendelea kuwekeza katika maeneo mbalimbali na kuwataka kuwapokea wawekezaji kutoka maeneo mengine ndani na nje ya nchi.

Aidha, amepongeza utekelezaji wa mkakati wa “Wilaya Moja Bidhaa Moja” ambao amesema ni mkakati mzuri unaoupambambanua Mkoa wa  Simiyu katika Sekta ya Viwanda.

“Nimeelezwa hapa na Mkuu wa Mkoa kuwa mmeanza kwa kila wilaya moja kuwa na bidhaa moja(kiwanda kimoja) lakini haikatazwi wilaya hiyo kuwa na viwanda vidogo, nimeelezwa kuwa Meatu mmeamua kusindika maziwa na Maswa kiwanda cha chaki, Bariadi kiwanda cha bidhaa za afya zitokanazo na pamba na hiki ni kiwanda changu ninacho kisimamia” alisema

“Nataka kuahidi kuwa kiwanda hiki kitajengwa na kitazalisha bidhaa za sekta ya Afya, Busega pia kitajengwa kiwanda cha maji tunayotundikiwa hospitali(IV Infussion/drip), Itilima nimeambiwa ni masuala ya asali na alizeti, lakini pia nimeambiwa kuna viwanda vya bidhaa za ngozi maeneo tofauti nawapongeza sana kwa mwamko mkubwa huu” alisisitiza Makamu wa Rais.

Wakati huo huo Mhe.Makamu wa Rais amewapongeza viongozi wa Mkoa na Halmashauri ya Mji Bariadi kwa kusimamia na kuhakikisha barabara za Mjini Bariadi zinajengwa kwa kiwango kinachoridhisha, hivyo amesisitiza usafi  uimarishwe katika barabara hizo hususani barabara iliyopewa jina lake  ili kupendezesha Mji.

Katika hatua nyingine Mhe.Makamu wa Rais amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Simiyu upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama ifikapo mwaka 2019/2020, kupitia Mradi mkubwa wa Maji kutoka Ziwa Victoria ambao unatekelezwa na Wizara iliyo chini ya Ofisi yake kwa kushrikiana na Wizara ya Maji.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema tarehe 21/02/2017Mhe. Makamu wa Rais atakutana na timu ya wataalam wanaofanya upembuzi yakinifu wa ujenzi wa Kiwanda cha bidhaa za afya zitokanazo na pamba mkoani humo,  ambapo alibainisha kuwa mkoa umejipambanua kwenye sekta ya viwanda hasa katika kutekeleza maono na mtazamo wa Viongozi wakuu wa Kitaifa.

Mbunge wa Bariadi Andrew Chenge akawasilisha changamoto za wananchi kwa Makamu wa Rais amesema wananchi Bariadi wanakabiliwa  na uvamizi wa tembo katika mashamba yao ,  hivyo ni vema ikawekwa mipaka na zikatafutwa njia ya kuwazuia, jambo ambalo Mhe. Makamu alilitolea ufafanuzi kuwa Serikali italifanyia kazi kuhakikisha wanyama hao hawawadhuru watu na kuharibu mazao.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe.Samia Suluhu Hassan akiwa katika ziara yake wilayani Bariadi ameweka Jiwe la Msingi Ujenzi wa Nyumba za Viongozi wa Mkoa wa Simiyu, amekagua ujenzi wa barabara za Bariadi Mjini na kufungua barabara moja iliyopewa jina lake”BARABARA YA SAMIA SULUHU”.

MWISHO 

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA HAPA:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/02/makamu-wa-rais-apongeza-viongozi-mkoani.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa