• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Makamu wa Rais Awahimiza Wananchi Kuchangia Ujenzi wa Miundombinu ya Elimu

Posted on: February 21st, 2018

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan amewahimiza wananchi mkoani Simiyu kuchangia ujenzi wa miundombinu ya elimu ili kuunga mkono jitihada za Serikali katika maendeleo ya Sekta ya Elimu.

Mhe.Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati  akizungumza na Wananchi wa Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu kwenye  Mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Nguzo Nane wakati wa ziara yake mkoani humo.

Amesema Serikali imeamua kutoa elimu bila malipo na kuwapunguzia wazazi mzigo wa kulipia gharama za karo na michango mbalimbali ya uendeshaji wa shule lakini suala la kuchangia ujenzi wa miundombinu ya elimu wananchi wanapaswa kuunga kuchangia ili kuunga mkono juhudi hizo.

“ Tunapeleka fedha katika shule zote za Msingi na Sekondari ili wanafunzi waweze kusoma vizuri lakini kwenye suala la ujenzi wa matundu ya vyoo, madarasa, maabara pamoja na kwamba Serikali ina wajibu wa kufanya hayo na ninyi wananchi mnao wajibu wa kusaidia kufanya hayo” alisema Mhe. Makamu wa Rais.

Wakati huo huo Mhe.Makamu wa Rais ameipongeza Wilaya ya Maswa kwa kuongeza ufaulu kutoka asilimia 45 hadi asilimia 75 kwa mwaka 2017 na akakemea vikali tabia ya wanaume wanaoua ndoto za watoto wa kike kwa kuwapa mimba , ambapo amesema jicho la Serikali liko kwa watoto wa kike na itawachukulia hatua kali wote watakaobainika kufanya hivyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt.Seif Shekalaghe amesema watoto wa kike 28 wameripotiwa kuwa na mimba katika kipindi cha mwezi Desemba 2017 hadi sasa na Serikali ya Wilaya kupitia Operesheni tokomeza Mimba imefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 15 na kati ya hao wawili wamehukumiwa miaka 30 jela kila mmoja.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini , Mhe.Stanslaus Nyogo amewashukuru viongozi wa Wilaya kuleta mafanikio katika elimu ikiwa ni pamoja na ongezeko la ufaulu.

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan mara baada ya kufungua Jengo la Upasuaji la Upasuaji Hospitali ya Wilaya ya Maswa ambalo limepewa jina lake “SAMIA SULUHU HASSAN OPERATING THEATER” amewataka Watumishi wa Afya kufanya kazi kwa bidii

Aidha, amesema Serikali itahakikisha inaboresha huduma za afya ikiwa ni pamoja na ujenzi wa vituo vya Afya katika kila kata na kuboresha huduma za Afya ya Mama na Mtoto ili kupunguza Vifo vya mama na mtoto.

Naye Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe.Josephat Kandege amesema Serikali imekusudia kujenga vituo vya Afya 286 kufikia  mwisho mwa mwaka 2017/2018  lengo likiwa ni kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa kupunguza mrundikano wa wagonjwa katika Hospitali za Wilaya.

Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi, Mhe.Mashimba Ndaki amesema pamoja na kuendelea kuboresha sekta ya Afya kwa kujenga miundombinu, ni vema Serikali ikaajiri watumishi wa Idara ya Afya kukabiliana na upungufu uliopo.

Mhe.Makamu wa Rais amemaliza Ziara yake Wilayani Maswa ambapo amefungua Jengo la Upasuaji la Upasuaji Hospitali ya Wilaya ya Maswa ambalo limepewa jina lake “SAMIA SULUHU HASSAN OPERATING THEATER” na kuzungumza na wananchi katika Uwanja wa Nguzo Nane.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI JUU YA TUKIO HILI:FUNGUA HAPA:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/02/makamu-wa-rais-awataka-wananchi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa