Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniania ambayo yamefanyika Kitaifa katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Maadhimisho haya yenye Kauli Mbiu “Kizazi cha Usawa Kwa Maendeleo ya Tanzania ya Sasa na ya Baadaye” yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali waliopo madarakani na wastaafu wakiwemo Mama Getrude Mongela, Mama Anna Abdallah, Spika Mstaafu wa Bunge la Tanzania, Mhe. Anne Makinda, Mwenyekiti wa UWT Taifa, Ndg. Gaudensia Kabaka, Katibu wa UWT Taifa, Ndg. Queen Mlozi na viongozi wengine
Katika maadhimisho hayo Mhe. Makamu wa Rais ametembelea mabanda ya Maonesho ya kazi mbalimbali za wanawake, mashirika, taasisi na wadau wa maendeleo wanaojihsisha na masuala ya wanawake na baadaye akapokea maandamano ya wanawake kutoka maeneo mbalimbali nchini.
PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/03/blog-post.html
Bariadi - Somanda
Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.
Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054
Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054
Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz
Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa