• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Makamu wa Rais Akitaka Chuo Kikuu Huria Kuongeza Udahili Kusaidia Tanzania Kufikia Uchumi wa Kati

Posted on: February 22nd, 2018

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amekitaka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kuongeza ubora na kupanua wigo wa udahili wa wanafunzi kwenye programu za sasa ili kuendana na Sera Tanzania ya viwanda na kufikia Uchumi wa kati ifikapo 2025.

Ushauri huo ameutoa katika mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria cha TANZANIA yaliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Makamu wa Rais amesema kuwa ili kuweza kufikia TANZANIA ya viwanda na kufikia uchumi wa kati 2025 lazima udahili wa wanafunzi katika vyuo vikuu ufikie kiwango cha angalau  asilimia 23.

“Naungana na Mhe.Rais kuwaomba muisaidie nchi yetu kuongeza kiwango cha udahili wa wananchi wake kwa haraka na kwa kasi itakayotuwezesha kufikia lengo la kuwa nchi ya Uchumi wa kati ifikapo 2025” alisema

“Kwa mujibu wa takwimu za Benki ya Dunia kiwango kidogo cha udahili katika elimu ya juu ni sifa ya msingi ya Uchumi wa chini na wa kimaskini, Uchumi wa kati na wa Viwanda hauwezi kufikiwa na kuwa endelevu pasipokuwa na kiwango cha udahili katika elimu ya juu  cha angalau asilimia 23” alisema Makamu wa Rais.

Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe.William Ole Nasha amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania katika maendeleo ya sekta ya elimu nchini kwa kuwa kimekuwa mtekelezaji mkuu wa malengo na mikakati ya Serikali kwa upande wa ujifunzaji kwa njia za masafa.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Profesa Elifas Bisanda amesema tangu Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kianzishwe idadi ya wahitimu imefikia 38, 993 baada ya mahafali ya 34 idadi hiyo imeongezeka kufikia 39,934, jambo ambalo limechangia  kukuza rasilimali watu hapa nchini.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu amesema kufanyika kwa  mahafali ya 34 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania mkoani humo kutakuwa chachu na kutaleta mwamko mpya wa elimu kwa wananchi Mkoani humo.

“Tuliona tuwaalike wanafunzi ili kujenga hamasa kwao, tulialika kamati zetu za shule, madiwani, walimu na wananchi wote wa Simiyu ili washuhudie tukio hili tukiamini kuwa kwa kuona tukio hili kila mmoja atatamani kuwa hivyo kesho,  kama siyo yeye basi awe  mwanaye au ndugu yake” alisema Mtaka.

Jumla ya wahitimu 941 kutoka Tanzania bara na Zanzibar na nchi jirani walihudhurishwa mbele ya Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda na kutunukiwa  Astashaha, stashahada, shahada, shahada za uzamili , ambapo miongoni mwa hao 941 wahitimu saba walitunukiwa  shahada ya uzamivu(PhD).


MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA HAPA:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/02/makamu-wa-rais-akitaka-chuo-kikuu-huria.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa