• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Makamu wa Rais Akemea Tabia ya Kupeana Zabuni za ujenzi wa Miradi Kindugu

Posted on: February 23rd, 2018

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan amekemea tabia ya baadhi ya viongozi kuwapa ndugu au jamaa zao zabuni za ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwepo miradi ya maji kwa kuwa ni kinyume cha taratibu na hali hiyo haiwatendei haki wananchi na Serikali.

Mhe.Makamu wa Rais aliyasema hayo jana katika kikao cha majumuisho alichokifanya mara baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku nne mkoani humo ambayo aliianza tarehe 19/02/2018.

Amesema miradi mingi hususani miradi ya maji katika maeneo mengi mkoani humo haitekelezwi kwa wakati na katika kiwango cha ubora unaotakiwa kwa kuwa baadhi ya viongozi wamekuwa wakipeana miradi hiyo kwa kuzingatia undugu/ ukaribu wao badala ya kuangalia sifa zinazotakiwa.

“Miradi mingi ya maji imeshindwa kwenye baadhi ya maeneo kwa sababu mmepeana kindugu ndugu, mnashindwa kukemeana mnashindwa kusimamiana miradi haiendi, msiwadhulumu wananchi haki yao; mlizoea huko nyuma mnachukua fedha za miradi na hamfanyi lakini siyo sasa hivi” alisema.

Mhe.Makamu wa Rais aliwaagiza Wakuu wa Wilaya kuwasilisha taarifa yenye orodha ya  miradi inayotekelezwa katika maeneo yao, mtu anayetekeleza, hatua iliyofikia, tarehe ya kumaliza mradi na ikiwa haijamalizika ioneshwe sababu za kutokamilisha miradi hiyo kwa wakati, lengo likiwa ni kutoa nafasi kwa vyombo vya dola kufanya kazi yake.

Aidha, amevitaka vyombo  vya dola ikiwemo Taasisi ya Kuzui na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) kufuatilia Miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri zote mkoani humo.

Sanjali na hilo Mhe.Makamu wa Rais amewataka viongozi mkoani Simiyu kufanya kazi kwa kushirikiana ili kuwaletea wananchi maendeleo katika maeneo yao.

Wakati huo Mhe.Makamu wa Rais amewapongea viongozi na wananchi Mkoani Simiyu kwa kufanya vizuri katika sekta ya Kilimo hususani Kilimo cha zao la pamba na akaahidi kuwa Serikali itahakikisha wakulima wanapata dawa za kuuwa wadudu waharibifu ili malengo ya kuongeza mavuno mwaka huu kufikia kilo milioni 300 yaweze kutimia.

Vile vile amewapongeza kwa kutekeleza Sera ya Tanzania ya Viwanda kwa kuanzisha viwanda katika maeneo mbalimbali kupitia Mkakati wa “Wilaya moja Bidhaa moja” ambapo amesema Serikali inakusudia kujenga Kiwanda cha Bidhaa za Afya zitokanazo na pamba (Bariadi) na Maji wanayotundikiwa wagonjwa(IV Fluid/Drip) katika wilaya ya Busega.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amehitimisha ziara yake jana Mkoani Simiyu ambapo alikuwa Mgeni Rasmi katika mahafali ya 34 ya Chuo kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

MWISHO 

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA HAPA:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/02/makamu-wa-rais-akemea-tabia-ya-kupeana.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa