Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan ameagiza Shirika la Mawasiliano nchini TTCL kufikisha mkongo wa Taifa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu ili vifaa vinavyotumika kutoa huduma vinavyowezeshwa na Mtandao wa Intanenti viweze kufanya kazi yake sawa.
Mhe. Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati akifungua Jengo la Huduma kwa Wateja la TTCL Mkoa wa Simiyu Machi 07, 2020 mjini Bariadi , ambapo amewahimiza watendaji wa TTCL kutoa huduma bora na kwa ufanisi.
Aidha, Mhe. Makamu wa Rais ametoa wito kwa wananchi kutunza na kulinda miundombinu ya mawasiliano na watakaobainika kuhujumu miundombinu hiyo watashtakiwa kama wahujumu uchumi.
Bariadi - Somanda
Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.
Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054
Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054
Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz
Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa