• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Majengo Yote Mapya ya Chama, Serikali yawekewe Miundombinu ya Kuvuna Maji ya Mvua:Dkt. Bashiru

Posted on: August 11th, 2019

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt.Bashiru Ally  amewataka wataalam wa ujenzi kuzingatia miundombinu ya uvunaji wa maji ya mvua katika usanifu wa majengo yote ya Chama na Serikali yanayoendela kujengwa hapa nchini, ili kupunguza gharama za uendeshaji zinazotumika kununua/kulipia maji  na kuwa na uhakika wa upatikanaji wa huduma ya maji katika majengo hayo.

Ameyasema hayo Agosti 10, 2019  wakati akikagua maendeleao ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Bariadi  na wakati akiweka jiwe la msingi ujenzi wa Ofisi ya CCM wilaya ya Busega mkoani Simiyu.

Amesema ikiwa majengo yote yatakuwa na miundombinu ya kuvuna maji ikiwa ni pamoja na kuwa na matenki imara ya kuhifadhia maji hayo, inapotokea maji yakakatika tunatumia maji yaliyovunwa lakini pia gharama za kuendesha ofisi hususani za kulipia huduma zinapungua.

“Naelekeza nchini nzima majengo yote mapya ya Chama kuanzia yale ya tawi, biashara na ofisi tuyasanifu kwa kuzingatia Miundombinu ya uvunaji wa maji ya mvua, na ndani ya Serikali nimemshauri waziri wa maji kuwa miongoni mwa mambo tunayotakiwa kuyafanya kukabiliana na changamoto ya maji ni ubunifu” alisema Dkt. Bashiru

Kuhusu zao la pamba amewataka viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuanzia ngazi ya tawi kuhakikisha wanafuatilia mwenendo wa ununuzi wa zao la pamba na kuwasilisha taarifa kwake lengo likiwa ni kuhakikisha wakulima wanapata haki yao.

“Sasa hivi Chama lazima kiwe mbele ya Serikali kutetea haki za wavuja jasho, nchi nzima machinery (watendaji wote ) ya chama lazima ifuatilie ununuzi wa mazao ya wakulima na mimi nipate taarifa za kila siku; maneno yamesemwa mengi tangu mwezi wa tano, mwezi wa sita na wa saba  tumekaa vikao mwezi huu wa nane ni vitendo” alisema.

Kwa upade wake Mbunge wa Busega Mhe. Dkt. Raphael Chegeni amemshukuru Katibu Mkuu wa CCM Taifa Dkt. Bashiru Ally kwa kuielekeza Serikali kuimarisha usimamizi wa suala la ununuzi wa pamba, ambapo hadi sasa limeanza kupata ufumbuzi kwa wanunuzi kupewa fedha na benki kwa ajili ya kununua pamba kwa wakulima kwa  bei elekezi ya shilingi 1200/=

Akitoa salamu za Serikali Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa wananchi wa Wilaya ya Busega kutumia faida ya kuwa na Ziwa Victoria kufanya shughuli za uvuvi kwa kutumia vizimba na mabwawa na wakati huo huo amewataka kujihusisha na kilimo cha umwagiliaji ili kujihakishia usalama wa chakula.

Akiwa Wilayani Bariadi, Dkt. Bashiru alitembelea eneo la ujenzi wa Tawi la Chuo cha usimamizi wa Fedha(IFM) kijiji cha Sapiwi na kupongeza viongozi na wananchi wa Kijiji hicho kwa kuwa na matumizi bora ya ardhi ya kijiji chao jambo ambalo limepelekea kijiji  kutoa eneo kwa ajili ya ujenzi wa chuo hicho ambacho kitawaletea manufaa wao kama jamii ya Sapiwi na Taifa kwa ujumla na kuwataka viongozi wengine kuiga mfano huo.

 Dkt. Bashiru yuko katika ziara yake ya kikazi mkoani Simiyu kwa ajili ya masuala mbalimbali ya Chama na kufuatilia suala la mwenendo wa ununuzi wa pamba.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/08/dkt-bashiru-majengo-yote-mapya-ya-chama.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa