• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Mabala Atoa Msaada wa Vitabu Simiyu

Posted on: November 7th, 2020

Mwandishi wa Vitabu Bw. Richard Mabala ametoa msaada wa  nakala 120 za vitabu vya fasihi vya "Hawa The Bus Driver" na "Mabala the Farmer " kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza na cha pili katika shule za Mkoa wa Simiyu.

Akikabidhi msaada huo  Novemba 06, 2020 kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Bariadi kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Afisa Elimu Taaluma Mkoa wa Simiyu, Mwl. Onesmo Simime amewataka wanafunzi hao kujisomea vitabu hivyo wapate maarifa yatakayowasaidia katika mitihani yao na maisha kwa ujumla ili kutimiza kusudi la mtoa msaada huo.

“Mvitumie vitabu hivi vizuri, mkijenga tabia ya kujisomea kuanzia kidato cha kwanza na cha pili mtakapofika kidato cha tatu na cha nne fasihi kwenu itakuwa rahisi kwenu; hakikisheni mnautumia msaada huu vizuri msome na siku moja akija Simiyu tutamleta awaulize maswali,” alisema Simime.

Akizungumza kwa niaba ya wakuu wa Shule, Mkuu wa Shule ya Sekondari Bariadi, Mwl. Ally Simba amemshukuru Mwandishi wa Vitabu Ndg. Richard Mabala ambapo amesema wameupokea msaada huo kwa mikono miwili huku akimhakikishia kuwa vitabu hivyo vitasomwa na wanafunzi na vitasaidia kuongeza ufaulu katika mitihani yao.

Nao wanafunzi wa Shule ya sekondari Bariadi wakizungumza kwa niaba ya wanafunzi wao wa mkoa wa Simiyu wameshukuru kupata msaada huo na kuahidi kuutumia kwa malengo yaliyokusudiwa.

“Tunamshukuru sana Mabala kwa msaada wake na tumeupokea kwa mikono miwilitunaahidi tutasoma kwa bidii vitabu hivyo na vitatusadia kujibu maswali ipasavyo ili tuweze kufaulu katika mitihani yetu,” alisema Kija Nyerere mwanafunzi wa kidato cha Kwanza Bariadi sekondari.

“Msaada huu una faida sana kwetu maana vitabu vinaelimisha, vinaburudisha naamini tutafanya vizuri katika mitihani yetu kwa sababu pia itatusaidia kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuachana na mila potofu,” alisema mwakilishi wa wanafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari Bariadi.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/11/blog-post.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa