• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa 2019 Simiyu Yafikia Asilimia 75

Posted on: July 19th, 2019

Naibu waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba ametembelea Viwanja vya Nyakabindi kujionea maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakatofanyika kuanzia Julai 28, 2019 hadi Agosti 08, 2019 katika Viwanja Vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu, ambapo ameridhishwa na maaandalizi hayo ambayo amesema kwa sasa yamefikia zaidi ya asilimia 75.

Amesema maandalizi ya mwaka huu ni tofauti na mwaka jana kutokana na mwaka jana kwa sababu mwaka jana yalikuwa ya dharura lakini mwaka huu  taasisi zimejipanga na baadhi ya zimeanza kujenga majengo ya kudumu katika Viwanja vya Maonesho.

“ Maandalizi ya mwaka huu ni tofauti na mwaka jana kwa sababu mwaka jana yalikuwa ni ya dharura lakini kwa udharura ule ule tulifanikiwa kufanya vizuri lakini mwaka huu, maandalizi yamekuwa tofauti kwa sababu majengo ya kudumu yameongezeka na niwahakikishie watu wote watakaokuja kwenye maonesho mwaka huu kupata vitu vizuri” alisema  Mgumba.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa wakulima, wafugaji, wavuvi na wadua wengine kushiriki katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 huku akiwahakikishia kuwa maonesho hayo yatakuwa makubwa sana hivyo wategemee matokeo makubwa pia.

Kwa upande wake Mratibu wa Nanenane kutoka Wizara ya Kilimo, Dkt. Kissa Kajigili amesema barabara zinazozunguka uwanja zenye urefu wa kilometa sita zimeshachongwa na visima vinne vya maji vinachimbwa kuongeza idadi ya viwili vilivyopo ili kuboresha  huduma ya maji katika viwanja vya  Nyakabindi.

Ameongeza kuwa Halmashauri zote 21 za Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga inayounda Kanda ya Nanenane ya Ziwa Mashariki na taasisi nyingine zimepanda vipando vya mazao mbalimbali kwa ajili ya kuwaelimisha wakaulima, wafugaji na wavuvi  ambavyo  vinaendelea vizuri.

Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yataanza tarehe 28 Julai, 2018 na yanatarajiwa kufunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan Agosti 01, 2019  na kufungwa Agosti 08, 2019 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/07/maandalizi-ya-maonesho-ya-nanenane.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa