• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Kongwa Wafanya ziara Mkoani Simiyu Kutembelea Miradi ya Vijana ili Kujifunza

Posted on: June 8th, 2018

Viongozi kutoka Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Deo Ndejembi pamoja na baadhi ya viongozi wa vikundi vya vijana wilayani humo wamefanya ziara Mkoani Simiyu ili kujifunza namna vikundi vya vijana vinavyotekeleza miradi yake.

Timu hiyo imefanya ziara ya siku mbili hadi Juni 08, 2018  katika miradi inayotekelezwa na vijana kwa kushirikiana na Halmashauri ambayo ni Kiwanda cha Chaki,  Kiwanda cha kutengeneza bidhaa za ngozi wilayani Maswa na Mradi wa kiwanda cha kusindika maziwa wilayani Meatu.

Mkuu wa wilaya ya Kongwa amesema wameamua kuja Simiyu kwa kuwa vikundi vyake vimeonekana vikifanya vizuri katika miradi yake, hivyo wamewaleta vijana wao ili wapate uzoefu na ari itawasukuma kubuni miradi yao na kujua namna bora ya kuiendesha.

"Tumeona tuje tujifunze kutoka Simiyu maana mkoa wa Simiyu umeonesha mfano wa namna vikundi vya vijana vinavyotakiwa kutekeleza miradi yake, tumeona kwenye vyombo vya habari na kwingineko mkipata sifa nyingi kutokana na miradi yenu kuonesha matokeo, nia yetu vijana waje waone wajifunze wapate hasira ya kufanya kitu cha kwao" alisema Ndejembi.

Ndejembi amesema ni matamanio yake kuona vijana wa Kongwa wanaanzisha miradi ya viwanda kama ilivyo kwa Maswa na Meatu kwa kuwa wilaya hiyo ndiyo inayofanya vizuri katika kilimo na ufugaji Mkoani Dodoma ambapo uzalishaji wa malighafi ya viwanda hivyo uko vizuri pia.

Ameongeza kuwa baada ya ziara hiyo vijana wake wamejifunza hivyo watakapofika wilayani Kongwa wataenda kufanya miradi ambayo itakuwa ya mfano na endelevu kwa kuwa tayari wana wafadhili waliokubali kutoa fedha kwa ajili ya kuanzisha miradi hiyo.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa, Dkt. Omary Nkullo amesema Halmashauri itahakikisha inatoa fedha kuwawezesha vijana kutekeleza miradi yao na itawasimamia ili waweze kufikia ndoto zao.

Akizungumza kwa niaba ya vijana kutoka Kongwa waliofika Simiyu kujifunza, Bw. Zamoyoni George amesema kuja kwao Simiyu hakutakuwa bure bali itakuwa chachu ya kuanzisha miradi endelevu na yenye tija ambayo hata vijana wa Simiyu wataenda kujifunza kwao.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe amewapongeza wilaya ya Kongwa kuona umuhimu wa kujifunza na kuwashauri kuwa fedha wakazozitoa kwa vijana kupitia asilimia tano za mapato ya Halmashauri, zielekezwe kutekeleza miradi ambayo italeta tija na kurejesha fedha za Halmashauri kwa wakati.

Aidha, Dkt. Shekalaghe amesema  Maswa itaendelea kuboresha ubora na biashara ya chaki (MASWA CHALKS)  na kuomba Wilaya ya Kongwa kuanza kununua Chaki za Maswa na kutumia katika shule zake, huku akisisitiza timu hiyo ya Kongwa pia kwenda kutangaza bidhaa za Ngozi zinazozalishwa Kijiji cha Senani wilayani humo.

Mkurugenzi wa Wilaya ya Meatu, Bw. Fabian Manoza akitoa maelezo juu ya  kiwanda cha maziwa amesema Halmashauri ina mpango wa kukipanua kiwanda hicho na Benki ya Maendeleo ya Kilimo imekubali kutoa mkopo wa shilingi bilioni 6 kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda hicho na kuboresha teknolojia ya uzalishaji ili kifikie uwezo wa kuzalisha lita 15,000 kwa siku kutoka lita 800 za sasa.

Mkoa wa Simiyu ni mkoa uliojipambanua kama mkoa wa Viwanda kupitia Falsafa yake ya “Wilaya Moja Bidhaa Moja Kiwanda Kimoja” ambapo umedhamiria kujenga uchumi wa viwanda kwa kutumia malighafi yake inapatikana hapa nchini.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU ZIARA HII YA WATU WA KONGWA FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/06/kongwa-wafanya-ziara-mkoani-simiyu.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa