• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Kilichojiri tamasha la pasaka Simiyu:Wananchi waomba matamasha mikoani yawe endelevu

Posted on: April 22nd, 2017

Wananchi mkoani Simiyu kwa mara ya kwanza wameshuhudia Tamasha la Pasaka na kuomba Mwandaaji wa Matamasha ya Nyimbo za Injili kuendeleza utaratibu huu wa kufanya matamasha wakati wa sikukuu mikoani.

Ombi hilo la wakazi wa Simiyu limetolewa wakati wa Tamasha la Pasaka mkoani  humo lililofanyika leo katika Uwanja wa Halmashauri Mjini Bariadi  na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi kutoka maeneo tofauti mkoani humo..

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao wamemshukuru Mwandaaji ya Tamasha hilo Mkurugenzi wa Msama Promotion Ndg.Alex Msama pamoja na viongozi wa Serikali Mkoani Simiyu kuona umuhimu wa kuandaa Tamasha hilo kwa kuwa nyimbo za injili zinazoimbwa na waimbaji mbalimbali wa Kitaifa na Kimataifa zinawafanya watu wasifu na kumwabudu Mungu na kuachana na mambo yasiyofaa.

“Tumelipokea kwa furaha sana tamasha hili na tunaomba leo isiwe mwisho kila mwaka liwepo; yaani kwetu ni kama zawadi maana tangu mkoa wetu uanze ni mara ya kwanza, hii ni dalili kuwa Mkoa wetu unatambulika na unapendwa,tunawashukuru viongozi wetu na tunamshukuru Msama kutuletea Tamasha la Pasaka” alisema Lilian Kagirwa mkazi wa Bariadi Mjini.

Naye, Daniford William mkazi wa Bariadi amesema wigo wa matamasha hayo utanuliwe na kuwawezesha wananchi katika mikoa yote nchini kupata ujumbe wa Neno la Mungu kupitia nyimbo za Injili katika nyakati tofauti kwa mwaka.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga akitoa salamu za Mkoa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka amesema Msama Promotion  afanye utaratibu wa kuandaa tamasha lingine kubwa mkoani Simiyu kwa kuwa wananchi hao wanampenda Mungu na wako tayari kumtukuza Mungu kupitia matamasha kama hayo.

“ Nichukue nafasi hii kuwakaribisha Msama Promotion na waimbaji wote wa nyimbo za injili mkoani Simiyu kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, huu ni mkoa mpya lakini ni mkoa wenye kasi kubwa ya maendeleo na niombe wakati mwingine mtuletee tamasha kama hili  siku ya Sikukuu ya Krismasi au Pasaka ili watu wengi wapate nafasi ya kumtukuza Mungu zaidi ya ilivyokuwa leo ”.

Aidha ,Mkuu huyo wa Wilaya amesisitiza wananchi kuendelea kuliombea Taifa na viongozi wote ili kudumisha amani, upendo na mshikamano wa nchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Msama Promotion, Bwana Charles Mwakipesile amewashukuru na kuwapongeza wananchi wa Bariadi kwa mapokezi mazuri na akaahidi kuwa Kampuni hiyo itakuza vipaji vya baadhi ya waimbaji wa nyimbo za Injili walionekana kuwa na uwezo mzuri kufanya vizuri katika medani ya muziki wa injili.

Tamasha la Pasaka Mkoani Simiyu limehudhuriwa na Waimbaji wa Kitaifa na Kimataifa wakiwemo Upendo Nkone,Beatrice Mwaipaja,Upendo Kilahiro, Martha Mwaipaja, Jesca Honore, Sifael Mwabuka na  kwaya mbalimbali kutoka katika Makanisa ya Mjini Bariadi.


Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa