• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Kila Mdau Awe Sehemu Kuufikisha Mkoa Namba Moja Mitihani Yote Kitaifa: RAS Simiyu

Posted on: December 10th, 2020

Katibu Tawala wa Mkoawa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga ametoa wito kwa viongozi, walimu, wazazi na wadau wote wa elimu mkoani hapa kushiriki kikamilifu katika kutekeleza na kuwezesha azma ya mkoa ya kuwa nafasi ya kwanza katika mitihani yote ya  Taifa.

Mmbaga ameyasema hayo Desemba 09, 2020 Mjini Bariadi wakati akifungua kikao cha viongozi, watendaji na wadau wa elimu mkoa cha kutangaza Mkakati wa Mkoa wa kuboresha taaluma kwa mwaka 2021 ambapo alibainisha kuwa endapo kila mdau atatimiza wajibu wake Simiyu itakuwa mkoa bora katika elimu.

“Mkoa wetu kushika nafasi ya kwanza inawezekana kabisa, kama tuliweza kutoka nafasi za mwishoni kabisha tukaingia, kumi bora, sasa hivi tuka katika tatu bora, naamini kwa uweza wa Mwenyezi Mungu tunaweza  kushika nafasi ya kwanza katika mitihani yote ya Taifa,” alisema Mmbaga.

Aidha, Mmbaga amewataka viongozi wa idara ya elimu kuepuka kutumia kauli chafu kwa walimu kwa kuwa zinawakatisha tamaa na kupunguza tija na ari katika utendaji kazi wao badal yake watumie mbinu sahihi za kiuongozi kutatua changamoto wanazoziona kwa walimu.

 Naye Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju amesema ushirikiano, mawasiliano na mahusiano mazuri baina ya walimu, viongozi na wadau wote wa elimu yanasaidia muda mwingi kutumika kufundisha na kusimamiana badala ya kutumika kuzozana, kugoma na kusuluhishana.

Baadhi ya walimu na Maafisa Elimu wa Kata na Halmashauti wamesema wameupokea mkakati huo na kuahidi kutimiza wajjibu wao ili kuweza kufikia malengo ya mkoa na kuboresha taaluma na elimu mkoani Simiyu huku wakitoa maoni mbalimbali namna ya kuboresha zaidi utekeelzaji wa mkakati huo.

“Nashauri mkoa uanzishe mitihani ya pamoja ya madarasa tarajiwa yaani darasa la tatu, darasa la sita, kidato cha kwanza na kidato cha tatu, mitihani hii itusaidia kujua shule zipi zina changamoto gani na itasaidia kuweka mikakati ya kuziwezesha kufanya vizuri kwa kuwa walimu na viongozi wengine watakuwa na mwaka mzima wa kuyaandaa madarasa hayo kabla ya mtihani wa Taifa,” alisema Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Lagangabilili Itilima, Mwede Hongoa.

“Tunaomba Serikali iboreshe makazi ya walimu, walimu wengi hawana nyumba za kuishi maeneo ya shule wengi wanatoka mbali na Shule hivyo wakati tunapohitaji kuwasaidia wanafunzi hasa nyakati za usiku inakuwa vigumu kwao kushiriki kikamilifu,” alisema Mwalimu Flora Shimbi Mkuu wa Shule Itilima Sekondari.

“Serikali ya Mkoa imetoa motisha kwa walimu hasa wanaofanya vizuri na walimu wa mkoa wa Simiyu wamehamasika sana na wanajituma katika kazi yao, tunaomba serikali iendelee kuboresha miundombinu ikiwemo vyumba vya madarasa, madawati na viti ili mazingira yao ya kufundishia yawe bora zaidi,” alisema Mwalimu Oscar Nsolo Mkuu wa Shule Sapiwi Sekondari.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo ameshauri mkoa wa Simiyu kuwa na mfuko wa elimu wa mkoa, ili mfuko huo uweze kusaidia katika ujenzi wa miundombinu ya elimu huku akitoa wito kwa wazazi na wadau wote wa elimu kuona umuhimu wa kuuchangia mfuko huo.

Mkakati wa kuboresha taaluma mkoa wa Simiyu kwa mwaka 2021 umejumuisha mambo muhimu ikiwa ni pamoja na Uwezo wa kujituma kwa viongozi wa elimu, uungwaji mkono na viongozi wa juu,uwajibikaji wa maafisa elimukata na mfumo wa utawala, huduma bora na mawasiliano kwa walimu/wadau wa elimu, utoaji wa motisha na zawadi, ufatiliaji kabambe wa ufundishaji na ujifunzaji, mafunzo kazini,upimaji, miundombinu na samani, kambi za kitaaluma, matumizi ya mitandao ya TEHAMA.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/12/kila-mdau-awe-sehemu-kuufikisha-mkoa.html

 

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa