• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

JPM Atoa Salamu za Pole kwa Majeruhi Sita wa Ajali Simiyu, Wakiwemo Waandishi Watano

Posted on: September 9th, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametoa pole kwa waandishi wa habari watano wa Mkoa wa Simiyu na Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika,Dkt. Titus Kamani waliopata ajali katika wilayani Meatu, wakati akiwa ziarani wilayani humo, salamu ambazo zimewasilishwa kwa niaba yake na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, ambaye aliwatembelea katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu walikokuwa wakipatiwa matibabu.

Akiwasilisha salamu za Mhe.Rais,  Mhe. Mtaka amesema magari matano ya Simiyu ya Serikali na gari binafsi yaligongana na watu sita wakajeruhiwa wakiwemo waandishi watano na Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika,Dkt. Titus Kamani  na kusisitiza kuwa Mhe. Rais ameguswa na jambo hilo, hivyo ametoa shilingi laki tano kwa kila majeruhi ili iwasaidie katika matibabu.

“...magari ya waandishi wa habari lakini kulikuwa na gari binafsi, baada ya msafara wa Rais kwa sababu ya vumbi,  dereva mmoja katika yale magari alisimama kutaka kuona njia vizuri, magari yaliyokuwa yakifuatana  matano yakagongana kwa nyuma, watu sita wakapata majeraha miongoni mwao walikuwepo waandishi wetu watano na Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika,Dkt. Titus Kamani”

“Mhe. Rais anatoa salamu zake za pole kwa majeruhi wote,  ameguswa sana na jambo hili hasa pale aliposikia kuwa sehemu ya majeruhi ni waandishi ambao tumekuwa nao pamoja katika ziara hii, wakafanya kazi kubwa ya kuuhabarisha Watanzania,  akaomba mimi kama Mkuu wa Mkoa nifikishe salamu zake za pole kwa niaba  yake kwa watu hawa sita” alisema.

Ameongeza kuwa Mkoa utaendelea kuchukua tahadhari kupitia jeshi la polisi hasa katika misafara ya viongozi na kuhakikisha kuwa wanajenga uelewa wa pamoja kwa madereva wakati wa maandalizi ya safari juu ya namna ya kuchukua tahadhari

.Rehema Evance ambaye ni mwandishi wa Azam TV amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwatambua na kuona awape mkono wa pole ambao amebainisha kuwa fedha hizo zitawasaidia katika kugharamia matibabu.

“ Kwanza namshukuru Mungu kwa kutujalia tukapona,  lakini kipekee napenda kumshukuru Mhe. Rais kwa kuona kuna haja ya kutusaidia katika hili, kwa hiki alichotoa Mungu ambariki sana kitatusaidia kwenye matibabu, tunaahidi kuendelea kuwahabarisha Watanzania na kuhakikisha yale yote yanayotendeka ndani ya nchi yanawafikia” alisema.

Ajali hii iliyotokea wilayani Meatu Septemba 09, 2018 imesababisha majeruhi sita ambao ni waandishi watano Rehema Evance (AZAM TV), Belensi China(ITV), Aidan Mhando(Channel Ten), Phaustine Fabian(Mwananchi), Mpiga Picha Samson Masunga pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika,Dkt. Titus Kamani na hakuna kifo kilichotokea..

Majeruhi wote walipatiwa matibabu katika Hospitaliya Wilaya ya Meatu ambapo waandishi wa habari Rehema Evance (AZAM TV), Phaustine Fabian(Mwananchi), Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika,Dkt. Titus Kamani waliruhusiwa na Belensi China(ITV), Aidan Mhando(Channel Ten), na Mpiga Picha Samson Masunga walipewa Rufaa kwenda Bugando kwa uchunguzi na matibabu zaidi.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/09/jpm-atoa-salamu-za-pole-kwa-waandishi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa