• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

JKT Kujenga Majengo ya Kudumu Uwanja wa Nanenane Simiyu Mwishoni mwa Mwaka 2018

Posted on: August 12th, 2018

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limewahakikishia viongozi wa Mkoa wa Simiyu kuwa litaanza kujenga majengo ya kudumu katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Bariadi mkoani humo, mwishoni mwa mwaka 2018.

Haya yamesemwa na Mwakilishi wa Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Martin Busungu, Luteni Kanali Respicious Kaiza wakati Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu na viongozi wa Wilaya ya Bariadi wakiagana na baadhi ya viongozi na Maafisa wa JKT katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi mara baada ya kukamilisha siku tatu za nyongeza za maonesho ya nanenane zilizotolewa na Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba, wakati akifungua maonesho hayo Kitaifa mwaka 2018, mkoani Simiyu.

Luteni Kanali Kaiza amesema viongozi wa JKT wameondoka Nyakabindi Uwanja wa Nanenane kwa lengo la kwenda kujipanga ili waondokane na majengo ya kuhamisha na kuanza ujenzi wa majengo ya kudumu katika uwanjauwanja huo katika maonesho yajayo.

"Tutaka kwenda kujipanga baada ya muda kidogo tutarudi kuanza rasmi ujenzi wa majengo ya kudumu ili tusiwe na majengo haya ambayo ni ya kuhamisha, Mungu akijalia mwishoni mwa mwaka huu tunataka tuwe tumeshaanza kujenga"'alisema.

Aidha, Luteni Kanali Kaiza amesema pamoja na viongozi na Maafisa wa JKT kuondoka Uwanjani hapo, vijana wa JKT pamoja na viongozi wa JKT waliokuwepo katika Kambi ya Nyakabindi wakati wa Maonesho ya Nanenane watabaki katika Eneo hilo la Nyakabindi kuendeleza shughuli walizozianzisha katika Uwanja huo.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema dhamira ya Mkoa huo ni kuwa na Maonesho ya Nanenane ya Kimataifa hivyo amewaomba viongozi wa JKT kuona uwezekano wa kujenga majengo makubwa zaidi ya yaliyotumika mwaka huu kwa kuwa mwaka 2019 watu zaidi ya 100,000 wanatarajiwa kushiriki maonesho ya nanenane na akawaomba pia waone uwezekano wa kuanza kujenga majengo hayo mapema kuanzia mwezi Oktoba, 2018.

Mtaka ametoa wito kwa JKT pia kujenga hoteli, hosteli, kumbi za mikutano na miundombinu mingine muhimu katika eneo la Nykabindi kwa kuwa eneo hilo litatumika kwa maonesho ya nanenane, maonesho ya kilimo biashara kila baada ya miezi mitatu na Vyuo vingi vya Elimu ya Juu vitajengwa karibu na eneo hilo, hivyo majengo hayo yakijengwa yatasaidia na kurahisisha kutoa huduma katika eneo hilo.

Aidha, amesema Serikali imeandaa utaratibu wa kuliendeleza eneo la Uwanja wa Nyakabindi ambapo itatoa nafasi kwa vijana, watumishi wa Umma walio tayari kufanya shughuli zao katika kilimo na mifugo kwa usimamizi wa Wataalam wa Kilimo na mifugo ili liweze kutumika kwa manufaa.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini ameshauri kwa kuwa JKT liwekeze katika ujenzi wa  hoteli na hosteli katika eneo la Nyakabindi  kwa kuwa ina nguvu kazi  ili watu wanapokuja kwenye maonesho wapate huduma ya malazi kwa urahisi ndani ya mkoa badala ya kutoka nje,  lakini pia JKT waweze  kufanya biashara kupitia uwekezaji huo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bw. Melckizedeck Humbe amesema uwepo wa JKT utachangia mji huo kukua kwa kasi, huku akibanisha kuwa Halmashauri inatarajia kupima viwanja katika eneo la Nyakabindi lengo ni kufanya JKT na wawekezaji mbalimbali kujenga miundombinu yote muhimu karibu na Uwanja wa Nanenane ikiwemo vituo vya mafuta, hoteli, kumbi na hosteli.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU TUKIO HILI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/08/jkt-kujenga-majengo-ya-kudumu-uwanja-wa.html

 

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa