• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Jeshi la Polisi mkoani Simiyu lakabidhiwa nyumba 10 za makazi ya askari

Posted on: October 15th, 2018

Naibu Katibu Mkuu wizara ya mambo ya ndani Ramadhani  Kailima amesema kwa kutambua tatizo la uhaba wa nyumba za makazi ya askari nchini tayari serikali imetenga shilingi bilioni 10 kwa ajili ya kujenga nyumba 400 katika mikoa  mbalimbali nchini ukiwemo mkoa wa Simiyu.

Naibu waziri Kailima ametoa kauli hiyo katika hafla ya uzinduzi wa nyumba 10 za makazi ya askari wilayani Maswa zilizokabidhiwa kwa jeshi la polisi na wakala wa barabara nchini -TANROAD  baada ya kukamilika mradi  wa ujenzi wa barabara ya Maswa – Shinyanga na kuongeza kuwa  katika awamu ya kwanza zitajengwa nyumba 148 kwa gharama ya shilingi bilioni 3.7 na awamu ya pili nyumba  252 kwa gharama ya shilingi bilioni 6.3 ambapo mkoa wa Simiyu utapata nyumba 20.

Aidha Mhe Kailima amewataka watendaji wote ndani ya jeshi la polisi kuzingatia maadili na kuepuka vitendo vya rushwa ambavyo amesema vinaichafua serikali na kupandikiza chuki katika jamii.

“ Tukio hili linaashiria namna ambavyo serikali inawajali askari wake, ninazindua nyumba hizi 10 kwa ajili yenu, sasa ni matumaini yangu makazi haya mapya yatawapa ari ya kufanya kazi kwa bidii zaidi bila upendeleo wala uonevu wa aina yeyote”, alisema mhe Kailima

Pia naibu waziri kailima ameliagiza jeshi la polisi mkoa wa Simiyu kuhakikisha linaweka utaratibu mzuri wa kuzitunza nyumba hizo sambamba na kuandaa mpango wa kuyampima maeneo yote yanayomilikiwa na jeshi hilo.

Akitoa hotuba kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Simiyu, mkuu wa wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga ameishukuru serikali kwa kutoa kipaumbele katika mgao wa nyumba hizo 10 kwa jeshi la polisi wilaya ya Maswa huku akiahidi kuendelea kusimamia nidhamu na uwajibikaji miongoni mwa watumishi umma mkoani Simiyu.

Naye Kamanda wa polisi mkoa wa Simiyu Deusdedit Nsimeki amewataka askari wote watakaopata nafasi ya kuishi kwenye nyumba hizo kuzingatia usafi na kuitunza vizuri  miundombinu yake  huku akiahidi kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kujiridhisha kama agizo lake linatekelezwa.

Jitihada za kuboresha makazi ya askari mkoani Simiyu zinatasaidi kudumisha hali ya amani na usalama halikadhalika kuongeza kasi ya kufikia malengo ya mkoa sambamba na ajenda ya taifa kufikia uchumi wa kati kupitia sekta ya viwanda.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa