• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

IGP Sirro: Jeshi la Polisi Halitawafumbia Macho watakaobainika kujihusisha na Mauaji ya Watoto Lamadi

Posted on: February 18th, 2019

Mkuu wa Jeshi la Polisi hapa nchini IGP Simon Sirro amesema Jeshi la Polisi halitawafumba macho wale wote watakaobainika kuhusika katika mauaji ya watoto katika Kata ya Lamadi wilayani Busega na badala yake litawashughulikia kwa mujibu wa sheria.

Inspekta wa Polisi Sirro ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Lamadi Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Kisesa Kijiji cha Lamadi, kufuatia matukio ya mauaji yaliyoripotiwa mwishoni mwa mwaka jana na hivi karibuni.

IGP Sirro amewatoa hofu wananchi wa Lamadi na kuwasihi kuendelea kuliamini jeshi la Polisi kuwa liko imara na kuwahakikishia kwamba Serikali yao ipo kazini kuhakikisha mauaji hayo yanakomeshwa.

Amesema mauaji hayo yamekuwa yakihusishwa na imani za kishirikina na ramli chonganishi hivyo akawataka waganga wa jadi wanaojihusisha na ramli chonganishi kuacha mara moja maana ni kinyume na sheria, huku akiwataka waganga ambao bado hawajasajiliwa kwa mujibu wa sheria wafanye hivyo haraka.

“Tutawashughulikia wote wanaotaka kuwafanya wana Lamadi wasiishi kwa amani, kwa sababu tunaamini waliofanya haya ni wanaopiga ramli chonganishi ambao ni wachache, nitumie nafasi hii kuwataka waganga ambao hawajasajiliwa kwenda kujisajili haraka, msipojisajili tutawachukulia hatua pia” alisema

Aidha, Sirro ametoa wito kwa jamii kuachana na imani za kishirikiana, mila na desturi potofu ambazo amesema zinarudisha nyuma maendeleo, badala yake akataka elimu iendelee kutolewa kwa jamii ili iweze kubadilika.

Katika hatua nyingine IGP Sirro aliwataka wananchi na viongozi Mkoa Simiyu kushirikiana na jeshi hilo, huku akisisitiza  kuwa ushirikiano watakaotoa kwa polisi ndiyo utasaidia wahusika wote kukamatwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  amesema kufuatia mauaji hayo Serikali imeshawafikisha mahakamani watuhumiwa wa mauaji ya watoto.

Aidha, Mtaka amebainisha kuwa kabla ya watuhumiwa kufikishwa mahakamani Serikali kupitia vyombo vyake vya dola ilisimamia zoezi la upigaji kura za siri ambazo wananchi waliomba wapige ili kuwabaini wauaji hao ambalo lilifanyika 13 Februari, 2019.

MWISHO.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa