• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Dkt Mwanjelwa Apongeza Simiyu Kujenga Jengo la Kudumu Uwanja wa Nanenane, Ashauri Kanda Nyingine Kuiga

Posted on: August 2nd, 2018

Naibu waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa amewapongeza viongozi wa Mkoa wa Simiyu kwa kujenga Jengo la Kudumu (Simiyu Exhibition Hall), katika Uwanja wa Maonesho wa Nanenane wa Kanda ya Ziwa Mashariki na akashauri  kanda zote za Maonesho ya nanenane kuiga mfano kwa mkoa wa Simiyu,  ili wananchi waweze kupata elimu endelevu katika teknolojia za kilimo.

Mwanjelwa ameyasema hayo katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Bariadi, wakati akikagua  jengo la maonesho la mkoa wa Simiyu ambalo limegharimu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 600 mpakakulikamilisha.

Aidha, amewapongeza viongozi wa mkoa wa Simiyu kwa jitihada za kuamua kujenga jengo hilo  katika Uwanja wa Nanenane ambalo litatumika kwa Maonesho ya Kitaifa na Kimataifa, ambapo watu kutoka mataifa mbalimbali kuja kuonesha bidhaa na tekonlojia zitakazowasaidia wananchi kwenda kwenye uzalishaji wenye tija.

“ Mahali hapa patakuwa ni sehemu ya kuwainua wakulima na wananchi kwa ujumla ili kupata uzoefu wa kilimo, hii itapanua wigo na uelewa wa wakulima wetu wa Tanzani, lakini nichukue fursa hii kuziomba kanda nyingine kuiga mfano wa Simiyu wa kuwa na majengo ya kudumu ya maonesho, yatakayotumika kila baada ya muda fulani si nanenane tu” alisema.

Katika hatua nyingine Dkt. Mwanjelwa amewashauri viongozi wa Mkoa wa Simiyu kuona namna kuhamasisha wafanyabiashara kujenga hoteli maeneo ya jirani na jengo hilo ili kujiandaa na huduma kwa watu watakaokuwa wakifika kwa ajili ya maonesho hayo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema mkoa utaendelea kufanya maonesho ya Teknolojia mbalimbali kila baada ya miezi mitatu katika Jengo hilo,  ili kuwapunguza kazi Watanzania kwenda nje ya nchi kushuhudia maonesho hayo lakini pia kuvutia mataifa pengine kuja nchini kuonesha teknolojia  mbalimbali za kilimo.

“ Baada ya nanenane maeneo mengi shughuli za maonesho huwa zinasimama, sisi tumejipanga kufanya maonesho ya teknolojia mbalimbali hapa na ndiyo maana pamoja na kujenga jengo hilo tumeamua kuweka miundombinu kama umeme, maji, vyoo vya kudumu , JKT nao watajenga majengo yao ya kudumu na ulinzi wa jeshi la polisi utakuwa wa kudumu pia” alisema.

“ Matarajio yetu kama Wizara mtakubaliana na sisi tungehitaji kuwa na Simiyu Agri-Exhibition (Maonesho ya Kilimo Simiyu) kila baada ya miezi mitatu, tunataka hiki kinachofanyika kwenye nanenane kijirudie miezi mitatu ijayo, ili wananchi wetu wapate mahali pa kujifunza teknolojia za kilimo biashara, usindikaji na kuongeza thamani katika mazao ya kilimo” alisema Mtaka.

Ameongeza kuwa katika maonesho hayo wakulima watapata nafasi ya kuona zana bora za kilimo, hivyo akatoa wito kwa waonyeshaji wa teknolojia za kilimo kutambua kuwa baada ya Nanenane watapata fursaya kuonesha tena teknolojia hizo.  

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI JUU YA HABARI HII FUNGUA KIUNGANISHI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/08/dkt-mwanjelwa-apongeza-simiyu-kujenga.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa