• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Darasa la Saba Simiyu Waahidi Kufanya Vizuri Mtihani wa Taifa

Posted on: September 10th, 2019

Wanafunzi wa darasa la saba katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu wamemuahidi Mkuu wa mkoa Anthony Mtaka hawatamuangusha katika mtihani wa Taifa Septemba 11-12, kwa kuwa wamejiandaa vizuri na wanaimani watafanya vizuri.

Wanafunzi hao wa shule ya msingi Somanda A na B wametoa ahadi hiyo kwa niaba ya wanafunzi wote wa darasa la saba wa mkoa wa Simiyu, mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthoy Mtaka wakati akizungumza nao na kuwatakia heri katika Mtihani huo.

Wamesema wana imani ya kufanya vizuri kwa sababu hata Mtihani wa Mkoa Utilimilifu(Mock) walifanya vizuri, wameandaliwa vizuri kwa kupewa mazoezi na mitihani ya mara kwa mara na wamepata mbinu na maarifa mapya ya kujibu maswali ya mitihani kupitia  kambi za kitaaluma zilizofanyika katika kila shule.

“Sisi tumejiandaa vizuri sana na nina uhakika tutafanya vizuri katika Mtihani wa Taifa kama tulivyofanya vizuri kwenye Mock, walimu wametuandaa vizuri tulikuwa na kambi ya kitaaluma ambayo imetusaidia kukutana na walimu tofauti waliotufundisha vizuri zaidi, tunamuahidi Mkuu wa Mkoa kuwa hatutamuangusha” alisema Luhinda Nalisha kutoka S/M Somanda A.

“Tumejiandaa vizuri na tumejipanga kufanya vizuri, pia tunamshukuru Mkuu wa Mkoa kuja kututembelea na kutupa mawaidha tutayafanyia kazi, shule ipo vizuri kitaaluma na nidhamu  hivyo tuna uhakika wa kufaulu mtihani wa Taifa” alisema Bugumba Nindwa mwanafunzi wa Shule ya Msingi Somanda B

Akizungumza na wanafunzi hao, Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewatakia mtihani mwema na kuwataka watumie mbinu walizopewa na walimu kufanya vizuri, huku akiwaonya  kutojihusisha na vitendo vya udanganyifu wa aina yoyote.

Katika hatua nyingine Mtaka ametoa wito kwa wahitimu wa vyuo vikuu  kufundisha masomo ya maandalizi ya Kidato cha kwanza(Pre-form one) kwa wanafunzi watakaohitimu darasa la saba  kwa ajili ya kuwaandaa wanafunzi na masomo ya elimu ya sekondari.

Naye Afisa elimu Msingi Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mwl. Christopher Ligonda akishukuru kwa niaba ya walimu amesema wanafunzi wameandaliwa vizuri na wamefundishwa vizuri na wako tayari kwa ajili ya mtihani na matarajio yao ni kupata ufaulu mzuri kama  walivyoahidi wenyewe.

Mkoa wa Simiyu una jumla ya wanafunzi 29,248  wa darasa la saba wanaotarajia kufanya mtihani wa Taifa Septemba 11-12, mwaka huu, ambao kati yao  wavulana ni  13, 594 na wasichana 15.654.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/09/wanafunzi-wa-darasa-la-saba-simiyu.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa