• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Daraja la Sibiti Kukamilika Machi 24, 2019

Posted on: March 15th, 2019

Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Albert Kent amesema Ujenzi wa Daraja la Mto Sibiti linalounganisha Mikoa ya Simiyu na Singida unatarajiwa kukamilika kwa awamu ya kwanza na magari kuanza kupita ifikapo Machi 24, mwaka huu.

Kent ameyasema hayo jana Machi 14, 2019 katika kikao cha bodi ya Barabara kilichofanyika Mjini Bariadi, kinachowashirikisha viongozi na wadau mbalimbali wakiwemo watendaji wa Wakala wa Barabara(TANROADS) na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA)Mkoani humo.

Kent amesema agizo la Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli la kuhakikisha wanakamilisha daraja hilo kufikia mwezi Machi, 2019 ambalo alilitoa wakati aipoweka jiwe la Msingi la ujenzi wa daraja hilo Septemba, 2018.

“Ujenzi wa Daraja la Sibiti awamu ya kwanza kama ilivyoagizwana Mhe. Rais utakamilika tarehe 24 mwezi huu,mkandarasi anaendelea na umaliziaji watutala barabara kwenye mwingilio wa daraja kubwa; taratibu za kuongeza kazi ili kukamilisha kuweka tabaka la lami kilomita 25 zinaendelea” alisema Mhandisi. Kent.

Katika hatua nyingine Kent ameeleza mapenddkezo ya bajeti kuwa TANROADS Mkoa wa Simiyu imependekeza na kuomba jumla ya shilingi 11, 461,470 kwa ajili ya matengenezo ya barabara zenye urefu wa kilometa 1008.76, madaraja makubwa 62 na madaraja madogo 50.

Naye Mratibu wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA), Mkoa wa Simiyu, Mhandisi.Salvatory Yambi amasema bajeti ya matengenezo ya barabara chini ya wakala huo Mkoani Simiyu ni shilingi 5,469,051,603.32 (Bajeti inayozingatia ukomo).

Nao baadhi ya wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara wametoa maoni yao juu ya kazi ya matengenezo ya barabara inayofanywa na TANROADS pamoja na TARURA kama ifuatavyo:-

“Tunaomba Serikali ione namna ya kuiongezea bajeti TARURA ili iweze kutekeleza majukumu yake vizuri maana na mtandao mkubwa wa barabara mjini na vijijini, itoke kwenye asilimia 30 na kufikia asilimia 40 na TANROADS wabaki na asilimia 60 kutoka kwenye asilimia 70 ya sasa” Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Bariadi, Mhe. Robert Lweyo

“ Sisi tumeanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Bariadi pale , tunaomba TARURA waweke kwenye bajeti yao fedha za ujenzi wa daraja la Mto Bariadi unaounganisha kata saba za Halmashauri yetu” alisema Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Mhe. Bahame Kaliwa.

“ Naishukuru sana TANROADS kwa kuweka taa katika Mji wa Lamadi, mmepafanya Lamadi papendeze na watu waweze kufanya biashara vizuri, ombi langu muone uwezekano wa kuweka taa katika Mji wa Nyashimo ambao ndiyo makao makuu ya Wilaya ya Busega”Mhe. Tano Mwera, Mkuu wa Wilaya ya Busega.

Naye Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amemtaka Mratibu wa TARURA Mkoa kuhakikisha agizo la Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. Pombe Magufuli la kujenga barabara ya kilometa tatu katika Mji Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mwanhuzi.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII TAFADHALI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/03/daraja-la-sibiti-kukamilika-machi-24.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa