• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

CUAMM Watoa Msaada Vifaa Kinga Kusaidia Kukabiliana na Corona Simiyu

Posted on: May 7th, 2020

Shirika lisilo la kiserikali la Doctor with Africa CUAMM linalofanya kazi na Mkoa wa Simiyu kama mdau wa Afya katika masuala ya UKIMWI na Huduma za Afya ya Mama na mtoto limetoa msaada wa vifaa kinga (viambukuzi) kwa ajili ya kuunga mkono Serikali katika kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona.

Akikabidhi msaada huo  Mei 06, 2020 mjini Bariadi kiongozi kutoka CUAMM Bi. Barbara Andreuzizi amesema  Vifaa kinga hivyo vina thamani ya shilingi  milioni nne ambapo amebainisha kuwa Shirika hilo pia limetoa msaada mafuta na gari litakalotumiwa na wataalam wa afya kutoa elimu ya tahadhari ya maambukizi ya Virusi vya Corona katika mkoa  wa Simiyu.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini ameshukuru CUAMM kwa kutoa msaada huo ambao ni sehemu ya makubaliano ya wadau wa afya na serikali mkoani humo katika kukabiliana na Corona na kuiagiza Timu ya mkoa ya usimamizi wa huduma za afya kuhakikisha vifaa hivyo vinapelekwa haraka katika vituo vya kutolea huduma za afya kwa wakati.

“Tatizo la COVID 19 liliporipotiwa kama mkoa tulikutana na wadau tukakubaliana  kujiandaa namna ya kukabiliana nalo katika maeneo ya utoaji elimu, vifaa kinga na vifaa tiba, tunawashukuru sana CUAMM kwa vifaa kinga hivi ambavyo naamini vitasaidia timu zetu za usimamizi wa Afya(CMT) za Wilaya na vituo vya kutolea huduma za afya,” alisema Sagini.

Aidha, Sagini amewataka wataalam wa afya ngazi ya  Mkoa wakiongozwa na Mganga Mkuu wa Mkoa kusimamia mafuta na gari lililotolewa na CUAMM kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi na kuhakikisha linafanya kazi iliyokusudiwa na elimu inawafikia wananchi inavyostahili mpaka maeneo ya vijijini.

 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Festo Dugange Simiyu inaendelea na jitihada mbalimbali kukabiliana na maambukizi ya virusi vya Corona ambapo amewashukuru CUAMM kutoa msaada wa vifaa kinga vitakavyosaidia  katika utoaji wa huduma kwenye vituo vya kutolea huduma za afya na kutoa wito kwa wadau wengine kuendelea kuunga mkono na wananchi kuendelea kuchukua tahadhari.

Naye Mratibu wa Mpango wa kukabiliana na Maambukizi ya Virusi vya Corona Dkt. Khamis Kulemba amesema msaada wa vifaa kinga, mafuta na gari kwa ajili ya kutoa elimu ni muhimu sana kwa kipindi hiki, ambapo amebainisha kuwa wataalam wa afya watashirikiana na Shirika hilo kuhakikisha elimu ya tahadhari ya Corona inawafikia wananchi na vifaa kutumika ipasavyo.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KINGANISHI HIKI KATIKA BLOG RASMI YA MKOA WA SIMIYU:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/05/cuamm-watoa-msaada-vifaa-kinga-simiyu.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa