• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

CRDB Yakabidhi Hundi ya Shilingi Milioni 60 Udhamini wa Nanenane Kitaifa 2020 Simiyu

Posted on: July 30th, 2020

Benki ya CRDB imekabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 60 kama mchango wa udhamini wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 yanayofanyika katika  Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu, Kanda ya Ziwa Mshariki inayoundwa na mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga kuanzia 01 Agosti, 2020 mpaka 08 Agosti, 2020.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Julai 30, 2020 Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa, Bw. Lusingi Sitta amesema benki hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia wakulima ambapo amesema benki hiyo imejipanga katika kuhakikisha kuwa wakulima wote wa pamba wanapata malipo yao kupitia akaunti za benki ya CRDB.

“Tumehakikisha kuwa AMCOS zote tumefungua nao akaunti kama CRDB tutahakikisha kwamba kila mkulima anayeuza pamba yake atalipwa kupitia akaunti yake ya CRDB na tumejipanga kwamba kila alipo mkulima wa pamba nasi tupo hapo ,” alisema Lusingi.

Aidha, Lusingi amesema CRDB imefungua tawi lingine katika Wilaya ya Meatu ambapo amebainisha kuwa benki hiyo imepeleka gari ambalo lina mahitaji yote muhimu katika utoaji wa huduma na wateja(wananchi ) hivyo wanaweza kupata huduma zote katika gari hilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga kwa niaba ya Wakuu wa Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga ameishukuru benki ya CRDB kwa kukubali kuwa mdhamini Mkuu wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2020 na kwa namna ambavyo imekuwa ikiwajali wateja hususani wakulima ambapo imetoa zaidi ya asilimia 60 ya mikopo kwa wanunuzi wa pamba msimu wa mwaka 2019/2020 ili pamba ya wakulima inunuliwe.

“Kuna maana kubwa sana kwa CRDB kudhamini maonesho ya nanenane kwa sababu, lengo la maonesho haya ni kuwasaidia wakulima wa kawaida kwenda kwenye ukulima wa kisasa, hivyo inapotokea CRDB inajitokeza kusaidia maonesho kufana, inaenda sambamba na lengo la nchi la kuinua wakulima wadogo wadogo kwenda kwenye ukulima wenye tija,” alisema Kiswaga.

Wakati huo huo Kiswaga amewahakikishia viongozi wa benki ya CRDB kuwa serikali itaendelea kufanya kazi na benki hiyo katika matawi yote huku akitoa wito kwa viongozi hao kutosita kuwaeleza viongozi wa serikali kila wanapohitaji msaada katika maeneo mbalimbali.

Katika hatua nyingine Kiswaga ametoa wito kwa wananchi kutoka mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga inayounda Kanda ya Ziwa Mashariki ya Maonesho ya Nanenane pamoja na maeneo mengine ndani na nje ya nchi; kujitokeza kwa wingi kushiriki katika maonesho ya Nanenane Kitaifa huku akiwahakikishia kuwa maonesho hayo yatakuwa ya tofauti kuwataka watarajia kuona teknolojia mbalimbali zinazoleta mapinduzi katika kilimo.

Kauli Mbiu ya Maonesho ya Nanenane mwaka 2020 ni “KWA MAENDELEO YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI CHAGUA VIONGOZI BORA 2020.”

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:https://simiyuregion.blogspot.com/2020/07/crdb-yakabidhi-hundi-ya-shilingi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa