• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Choroko Zilizonunuliwa Nje ya Mfumo wa Stakabadhi Ghalani Zipelekwe Ghala Kuu: RAS Simiyu

Posted on: February 28th, 2021

Wafanyabiashara wa choroko mkoani Simiyu wametakiwa kuwasilisha choroko zote zilizokusanywa kutoka kwa wakulima nje ya utaratibu wa mfumo wa stakabadhi ghalani na kuzipeleka katika ghala kuu kwa ajili ya kuingia katika utaratibu wa mauzo kwa njia ya mnada.

Rai hiyo imetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga katika kikao chake na baadhi ya viongozi, watendaji na baadhi ya wafanyabiashara wa choroko, kilichofanyika jana Mjini Bariadi.

"Mfumo unaotakiwa kufuatwa katika ununuzi wa choroko kwa manufaa ya mkulima kupata bei nzuri ni mfumo wa stakabadhi ghalani, wanaosimamia mfumo huu wahakikishe kwamba mwongozo huu unazingatiwa kwenye malipo ya wakulima ambao unawataka kufanya malipo kwa wakulima saa 48 baada ya mnada kufanyika," alisema Mmbaga.

Katika hatua nyingine Mmbaga amezitaka Halmashauri zote mkoani hapa kuimarisha usimamizi na kuhakikisha Wafanyabiashara na wote wanaohusika na biashara ya choroko kulipa kodi na tozo zote zilizoainishwa katika mwongozo kutoka kwa Mrajisi wa Vyama vya Ushirika nchini, huku akisisitiza wadau wote kuzingatia mwongozo huo ili kuepuka hasara isiyo ya lazima.

Ameongeza kuwa mwongozo wa mfumo wa stakabadhi ghalani usimamiwe ili wadau wa zao la korosho wakiwemo wakulima na wanunuzi kila mmoja apate stahili zake na kubainisha kuwa watakaokiuka watakuna na mkono wa sheria.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Itilima, Bi. Elizabeth Gumbo amesema wao kama watekelezaji maelekezo ya ununuzi wa choroko yaliyotolewa na Katibu Tawala wa Mkoa, Bi. Miriam Mmbaga yanatekelezwa kwa kuzingatia mwongozo uliotolewa na kuwaasa wafanyabiashara kutokiuka sheria na mwongozo huo kwa kuwa watakapokiuka watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria..

Naye Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Simiyu, Bw. Ibrahim Kadudu amesema umuhimu wa utaratibu huu utamnufaisha mkulima katika bei ambapo badala ya choroko kununuliwa kwa kwa bei holela na ya kificho lakini kupitia mfumo huu wakulima watalipwa kwa bei ya ushindani ambayo kwa sasa kuwa mnada uliofanyika Februari 25, 2021 katika mikoa ya Mwanza na Shinyanga bei ilikuwa shilingi 1650.

Ameongeza kuwa mfumo wa stakabadhi ghalani utaisaidia Serikali kupata takwimu sahihi zitakazosaidia katika mipango ya kilimo kwa kuwa wakulima watakuwa wakipeleka choroko zao kwenye AMCOS kabla ya kuzipeleka katika maghala makuu kusubiri mnada hivyo takwimu za wakulima na mile walichozalisha kitapatikana kwa usahihi na kwa urahisi.

Mfumo huu pia utazisaidia Mamlaka za Serikali za Mitaa kukusanya mapatokwa kuwa baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu wamekuwa wakisafirisha choroko kwa njia za panya na kukwepa kulipa ushuru na tozo zilizowekwa kisheria.

MWISHO

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa