• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Bodi ya Ushauri ya Hospitali Teule ya Mkoa wa Simiyu Yazinduliwa Rasmi

Posted on: July 1st, 2018

Bodi ya Ushauri ya Hospitali Teule ya Mkoa wa Simiyu imezinduliwa rasmi na kutakiwa kusimamia vema Hospitali hiyo ili kuhakikisha huduma za afya zinatolewa ipasavyo kwa wananchi.

Akizungumza katika uzinduzi huo ambao ulifanyika katika Ukumbi wa Hospitali hiyo Mjini Bariadi, mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini, Katibu Tawala Msaidizi anayesimamia Utawala na Rasilimaliwatu Chele Ndaki,  amesema bodi hiyo inalo jukumu kubwa la kuisimiamia hospitali teule ya mkoa na kuhakikisha huduma za afya zinatolewa katika viwango vinavyotakiwa.

"Mnalo jukumu kubwa katika kuhakikisha kwamba huduma za afya zinazotolewa zinaendana viwango vya Serikali yetu, nafikiri hata ninyi mnaona namna viongozi wetu walivyolipa kipaumbele suala afya, lengo ni kuhakikisha wananchi ambao ndiyo waajiri wetu wapewe huduma nzuri na waendelee kufanya shughuli zao za uzalishaji" alisema Ndaki.

Amesema pamoja na kushauri juu ya namna hospitali inavyotoa huduma, bodi hiyo pia itakuwa na jukumu la kushauri uongozi wa hospitali na kutoa mapendekezo juu ya mambo mbalimbali yanayolenga kuboresha mazingira ya utendaji kazi kwa watumishi ili waweze kutoa huduma zinazotakiwa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Hospitali Teule ya Mkoa wa Simiyu, Bw. Gigi Mathias amesema wajumbe wa bodi hiyo wamejiwekea mpango kazi utakaowazesha kutoa ushauri ili kuboresha mambo mbalimbali katika hospitali hiyo.

"Kama bodi tutaishauri Menejimenti ya Hospitali iweze kuboresha huduma kwa wananchi na watumishi pia kwa sababu kama watumishi hawataboreshewa huduma zao muhimu utendaji wao utakuwa hafifu; tutasimamia rasilimali zote za hospitali,  pia tuna jukumu kama bodi kusimamia kandarasi zote na kuhakikisha zinafanya kazi  kwa viwango” alisema Gigi.

“Kwa kuwa bodi hii ina wajumbe wengi ambao ni watumishi wa Serikali na wengine ni wastaafu ambao ni wazoefu katika nyanja mbalimbali nina uhakika tutaishauri Menejimenti ya Hospitali Teule ya Mkoa wa Simiyu katika masuala yote kwa lengo la kuboresha utendaji na utoaji wa huduma bora" alisisitiza.

Naye Mjumbe wa bodi hiyo Bw. Said Zongo amesema wajumbe wa bodi hiyo watafanya kazi ya kuishauri Menejimenti ya Hospitali Teule ya Mkoa kwa mujibu wa sheria na taratibu.

MWISHO.




Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa